8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
1/20
ISSN 0856 - 3861 Na. 1232 SHAABAN 1437, IJUMAA , JUNI 3 - 9, 2016 BEI TShs 800/=, Kshs 50/=
Sauti ya Waislamu
www.annuurpapers.co.tz au facebook:[email protected] AHLU SUNNA WAL JAMAA HAJJ AND UMRA TRUST
Walio chinjwa Mwanza
Mazito yazidi kuibuka
Swadakta AskofuDavid Mwasota
Amesema kweli Msemaji wa PolisSheikh wetu Mwanza unapotosha
Baada ya kukosa Urais…
Maalim anaelekea wapi?Hata hivyo, alikuwa na daima atakayekuwa
Wasomi Saudia wazinduka usingiziniWaziri Mwinyi, huwezi kupigana na kivuli
WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mh. Dkt. Hussein Mwinyi.
Mtume(saw) amesema, “Mwenye kujakunizuru mimi kwa kutaraji ujira kwa Allahbasi mimi nitakuwa muombezi na shahidwake (siku ya Kiama)”. Wahi sasa kuja kulipujihakikishie kuombewa na Mtume wako(saw)Gharama zote kwa Hijja 2016/1437 ni Dola4,600. Umra ya Ramadhani ni Dola 2,700Karibuni Ahlu Sunna wal Jamaa kwa hudumanzuri na uongozi bora. Wasiliana nasiTanzania Bara: 0679895770/ 06888957770765462022; 0712735363. Zanzibar
0777468018; 0777458075; 07778450100777497300.
(11) UOMBEZI WA MTUME(SAW
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
2/20
2 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 201Mafundisho ya Qur'an/Uwanja wa Maarifa
Fethullah-Gulen
“Wale ambao wameaminina wakahama nawakapigana katika njiaya Mwenyezi Mungukwa mali zao na nafsi
zao wana daraja kubwasana mbele za MwenyeziMungu na hao wao ndiyowenye kufuzu” [AT-TAWBA 20]
Mara zote katikaQur’an tukufu inatangulia jihadi kwa mali kablaya jihadi kwa nafsiisipokuwa katika ayamoja au aya mbili. Ndiyopanadhanishwa kwangukwamba binadamu mudawa kuwa yuhai, anaifanya bora na anaitukuza maliyake juu ya maisha yakewakati wote. Na katikahali hadithi tukufuinasema: “Mwenyekuuliwa nyuma ya maliyake huyo ni shahidi”.Kwa upande mwingine,hadithi inatufundisha
hukumu maalumukwenye haya maumbileya binadamu. Na huukuwa mfano mbele zetukwamba mali na nduguwa karibu sana wa rohoni mtihani.
Kuna watu wameiachadunia kwa moyo, sikwa matendo au kwakuchuma. Katika watuhao ni Abubakar naUthman na Abdi-Rahman Bin Auf (r.a.).Na kuna watu ambaohawakumiliki maliyoyote katika dunia tokeamwanzo. Katika hali yawatu hawa inakuja nafsikabla ya mali. Hili kitabiani pindi watakapokuwa
hawakufikia kwenyekupata badala ya hakikaya hizo nafsi.
Ndiyo, si rahisi kamainavyokuja harakakwenye akili, kuaminina kutenda yale yoteyanayo hukumuliwa naimani hii. Kwani maishani mkusanyiko wa hisiana utambuzi wa mazoeaambayo yamejengekana yakijengeka katikaujumla wa miaka mingiwakati yanapoongezwakwenye mambo hayo yamaumbile, kunakuwa
vigumu sana juu ya binadamu kujitoamuhanga kwa mali yakena nafsi yake. MchukueniBwana wetu Hamza
(r.a.) Ammi ya Mtume(s.a.w.) na ndugu yake wakunyonya – kwa hakikaalizingazinga katika baadhi ya wakati kabla yakutangaza imani yake. Na badala ya kuwakasirikiawale ambao hawauvukimtihani mgumu katikamaudhui ya kujitoamuhanga kwa mali nanafsi na huo ni mtihanimgumu kwa watu wote.Ni juu yetu tuonyesheumuhimu mkubwasana kwa watu haona kuwasaidia kwakuwaombea kwa njia yasiri.
Ndiyo, kulikuwakuamini ni kuvukakikwazo cha kwanzacha shetani. Kwa hakikakuacha mtu jamaa zakena kabila lake na mkena watoto wake nandugu zake na kuhamakwenda mji mwingine,hiki ni kikwazo kinginecha kwanza. Hakikahakusimama kwakuihama nchi na mjikisha kutotosheka na hilotu, bali kupigania diniya Mwenyezi Mungukatika mahali papya,kunahesabiwa ni kuvukakikwazo chenginekigumu. Na mwenyekuwezeshwa katika jambo hili, kwa hakikaameidhibiti nafsi yake naamefika kwenye uokofu.
Surat Tawba aya ya 20
Leo ni Tarehe 27 Shaaban mwaka 1437 AH, sawa na tarehe 3 Juni, 2016. Tarehe6 June tunategemea kuangalia mwezi kwa Ramadhan na Tarehe 7 June 2016tukijaaliwa tutaanza Ramadhan Rasmi. Kutokea hii leo Ijumaa ya tarehe 27 May2016 hadi kufika kuanza mfungo wa Ramadhani tumebakisha siku 3.
Mwandamo wa mwezi
Jee Unajua?
CHEMSHA BONGO: 54Weka duara kwenye jawabu ilio sawa. Jawabu kamili wiki ijayo
UWANJA WA VIJANA-JIONGEZEE MAARIFA
JAWABU CHEMSHA BONGO NAMBA:53
MASAUALA1. Itaje Sura na Aya ya ngapi isemayo “Kwani haikukujieni khabari ya walio
kufuru.” Jawabu: 64:52. Itaje Sura na Aya ya ngapi isemayo “Hakika tumewajaribu hawa kama tulivy
wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapokuwa asubuhi.” Jawabu: 68:17
3. Itaje Sura na Aya ya ngapi iemayo “Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa. Jawabu: 74:6
4. Mara ngapi katika mwaka Malaika Jibril akitalii Qur’an na Mtume Muhamma(SAW)? Jawabu: Mmoja
5. Nani aliokuwa Muadhini wa mwanzo katika Uislamu? Jawabu: Bilal6. Kabla ya Vita vya Badr , Sahaba gani alitoa kauli ya kumuunga mkono Mtum
Muhammad (SAW) kwa maneno yafwatayo “ Ewe mjumbe wa Allah, sisi sio kam
wale watu wa kaumu ya Mtume Mussa AS walionena “Wewe na Mola wako na Molawako watapigana nasi tunakungoja hapa”, “Sisi tutakuambia nenda popote pale Allaalipokuamrisha, Tunaapa kuwa aliokutuma kwa haki basi sisi tutakuwa na wewe begkwa bega, tutapigana upande wa kulia, wa kushoto, usoni na nyuma, hatutokimbia
Jawabu: Muadh bin Jabal7. Taja idadi ya Waislamu na Wakiristo pale Tariq bin Ziyad alipoongoza kampeni y
kupambana na wasio Waislamu nchini Spain? Jawabu: Waislamu 1,000 Wakiristo 3,008. Syd Umar bin Khatab aliuanzisha mji upi kati ya hii: Fustat, Kufa, Basra
Jawabu: Kufa9. Mahujaji wanapotoka Arafa huelekea wapi kwa usiku mmoja? Makka, Muzdalifa
Mina? Jawabu: Muzdalifa10. Mwaka gani Syd Umar bin Khatab alisilimu, 610, 608, 622 AD? Jawabu: 610
MASUALA1. Itaje Sura na Aya ya ngapi isemayo ‘’ Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?2. Itaje Sura na Aya ya ngapi isemayo “Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko3. Itaje Sura na Aya ya ngapi isemayo ‘’ . Hakika walio wafitini Waumini wanaumna Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu nwatapata adhabu ya kuungua. ‘’4. Mwezi gani kati ya mwaka ndio imeteremshwa Qu’ran.5. Usiku upi uliobora koliko miezi alfu.6. Tafsiri ya Qur’an kutoka Kiarabu kwa Kiengereza iliomaarufu ni ya msomi gani?7. Al Khawarizmi alikuwa mvumbuzi wa somo gani?8. Utawala wa Abassid uliweka makao makuu yake wapi?9. Utawala wa Umawiyah uliweka makao makuu yake.10. Shairi maarufu la Rubaiyat limeandikwa na msomi gani wa Kiislamu alio maarufu
1. Silaha zenye kuuwa ni nyingi kati ya hizo zilizohatari kabisa ni Flamethroweiliotumiwa kwa mara ya kwanza katika vita vikuu vya Dunia, huu ni motunaosambazwa na bunduki kubwa, kisha kuna Light weight machinegun, Napalm bom
likipigwa huigeuza hali ya joto kufikia nyuzi 1200 degrees Celsius, buduki ya AK-5hp://www.therichest.com/buzz/10-of-the-deadliest-weapons-in-the-world/?view=all2. Tovuti ya Web com na Weebly ndio mjarab kuzitumia ukiwa unataka kuanzishtovuti yako kwa kazi mbalimbali: hp://www.top10bestwebsitebuilders.com/weeblyvs-web?utm_campaign=T104&a=T104&utm_source=taboolaNI&utm_medium=nationalinterest&ts=taboo&taboola_campaign=2177553. China inaongoza kwa matumizi ya Plastiki na kuwapiga kumbo nchi za Ulayhps://euobserver.com/china/1138064. Viwanda vya Plastiki nchini Marekani vinachukua namba ya tatu, hii inaonyeshmatumizi makubwa ya Plastiki kwa nchi hio: hp://www.firstamericanplastic.com
blog/10-facts-about-us-plastics-industry5. Nchi ya China inaongoza uzalishaji wa nyama duniani kwa mwaka husafirish74,538,698 m/t (metric tones) ikifwatiwa na nchi ya Marekani yenye kuzalisha 43,171,48m/t: hps://top5ofanything.com/list/c215cc3c/Meat-Producing-Countries6. Nchi ya Marekani inazalisha asilimia 19 ya nyama yote inayozalishwa duniani: hp:
beef2live.com/story-world-beef-production-ranking-countries-0-1068857. Rikodi iliopo juu ya mtu aliohifadhi Qur’an msahafu wote ni kijana wa umri wmiaka 3 aitwaye Abdulrahman Farah kutoka nchi ya Algeria: hps://www.youtubcom/watch?v=fghyJHl0Q608. Inaelezwa kuwa nchi ya Saudi Arabia inasambaza Misahafu milioni 30 duniani kotkila mwaka: hp://www.economist.com/node/103113179. Idadi ya Waislamu duniani ni Bilioni 1.2 inakisiwa kuwa kuna watu wafikamilioni 8 wamehifadhi Qur’an yote: https://answers.yahoo.com/questionindex?qid=20070911215529AA8RPX510. Ulaya imepigwa na wimbi kubwa la Makanisa kuwa hayatumiki na kununliwna Waislamu na kugeuzwa kuwa Misikiti: hp://www.gatestoneinstitute.org/276converting-churches-into-mosques
M W W M M B N 64:5 H F A A M
M A A U A A A 608 AD A U L B U
O I K Z Y S J 10:16 K S I U A
J S I D A R A 4:4 U T A B D
A L R A H A F 35:5 F A B A H
G A I L U B D 68:17 A T U K Bin
A M S I D A E 610 AD F Y T A J
N 1,000 T F I G R 74:6 U A A R A
C D O A 10,000 H N 6:8 S T L K B
B O 3,OOO N D A 5:22 T H I Y A
B I L A L A H 2:99 A R B A L
A J M R D O 78:9 L A B M I A
B O A A A M 7:5 A L A A L L
D R J M M A 4:12 L M G G H G
A D T A A R 5:5 A A H H A E
L A B D S K 666 U A D R M B
L N E H C H T L T A I Y R
A C B A U A K Q K D B A A
Y. A N N S Y 77:12 A U Y S Q
A I D K L A 85:10 D B U I I
L R T A U M Y R R N R B
I O M A S B A I H Y U J I
MKURUGENZI wa PANITA, Dkt. Tumaini Mikindo wa Jukwaa la Lishe Tanzania akiongeana viongozi wa dini (hawaonekani pichani) katika semina ya masuala ya chakula na lisheiliyofanyika katika Hoteli ya Protea Jumanne wiki hii, jijini Dar es Salaam.
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
3/20
3 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 201Maoni yetu
KUFUATIA tukio la kuuliwaWaislamu katika Msikitiwa Rahman, jijini Mwanza,gazeti la Kikristo, Jibu laMaisha linaripoti kuwaviongozi wa madhehebu zaKikristo wameungana nawenzao wa dini ya Kiislamukukemea na kulaani mauwajihayo.
Katika waliotoa kauli niKatibu Mkuu wa Umojawa Makanisa ya PentekosteTanzania (CPCT), AskofuDavid Mwasota. Ziponukta tatu za msingi sanaza kuzingatia katika mengialiyosema Askofu David.Kwanza anasema kuwa hilini jambo lenye mtandaowa kimataifa, kwambalinagusa dunia nzima. Pili,akatahadharisha kuwawaumini wa dini zotewaepuke “kutoa matamko
ambayo yanaweza kutoamwanya kwa adui kuendelezamaovu yake.” Tatu, akasema,tena kwa msisitizo maalum,kwamba:
“Serikali ipo kazini,haijalala, ukweli utajulikana,hayo madai mengine ni kamakumpa adui nguvu zaidi.Yatupasa kuungana pamojakumbaini adui.”
Sisi tunasema, SwadaktaAskofu David Mwasota.Maneno haya ya AskofuMwasota, yanatukumbushaile kauli ya Maaskofu waKanisa Katoliki nchini baada
ya tukio la kuuliwa PadiriEvarist Mushi kule Zanzibartarehe 17 Februari, 2013,na kutokea baadhi ya watukuanza kusambaza fitnakupitia vipeperushi na kauliza mitaani, wakichocheachuki na uhasama wa kisasi
baina ya Waislamu naWakristo. Maaskofu walewaliwataka waumini waona Watanzania kwa ujumlakutulia, na kupuuza fitnahizo, bali waiache serikali navyombo vyake kufanya kazi.
Ni kweli kabisa kama
alivyosema Askofu DavidMwasota, hili sio tukio lakutizamwa ki-Mwanzaau Kitanzania. Ni jambolililogubikwa na vurugu nasiasa chafu zinazoendeleaulimwenguni hivi sasa.Lakini muhimu zaidikama alivyotahadharishani kuwa, mkianza kusemaovyo mkitoa kauli zakuwafitinisha wenyewe kwawenyewe, mnampa aduinguvu kuwavuruga zaidi.Mnakabana makoo kwa
Swadakta Askofu David Mwasota Amesema kweli Msemaji wa PolisiSheikh wetu Mwanza unapotosha
mambo ambayo pengineyanafanywa na adui wakupanga kutoka nje au wandani anayetumiwa kamakibaraka na msaliti, lakini surainayopakwa ni kuwa ni nyinyikwa nyinyi mnaoparurana.
Mfano chukua kaulikama hii ya Sheikh Hassan
Kabeke wa Mwanza.Sheikh huyu amenukuliwaakiwatahadharisha Waislamukuepuka ‘imani za kisasa’zinazohamisha mauwaji.Sheikh Hassan Kabekeamesema “mauwaji hayoyamewadhalilisha Waislamukutokana na kuuingizaUislamu kwenye matatizoakiwataka waumini wa dinihiyo kurejea kwenye Uislamuwa asili wa Imani hiyo.”
Limeripoti gazeti la JamboLeo la Jumatatu wikihii likikariri kauli ya SheikhKabeke wakati wa dua yakuwaombea marehemuiliyoandaliwa na Taasisiya Bilal Muslim Mission ofTanzania.
“Leo sifa yetu imetiwadoa na watu wachache.Tumedhalilika na kuchezewakwa sababu tumeachaUislamu wetu wa asili.”
Haya ndiyo mfano wamaneno anayosema AskofuDavid kwamba ‘tukiropokaovyo’ yanampa mwanya aduikuendeleza maovu yake na
kutubamiza zaidi.Kwanza labda tuulize,
Uislamu wa kisasaunaoruhusu watu kuwachinjawenzao msikitini au mahalipengine popote, ni upi?Kama kuuwa ni haramu.Imepigwa marufuku katikaUislamu, utamuhusishajemtu anayechinja watumsikitini na Uislamu? Na hatalikitokea tukio kama hilo namuhalifu akajinasibu kuwani Muislamu na anafanyahivyo kutekeleza Uislamu,lazima jambo kama hilolitizamwe kwa mapana yake.Itikadi na fikra potofu kamahizo, huwa zinapandikizwakutoka mbali na watuwenye malengo ya mbali namara nyingi watekelezajiwanakuwa ni vibaraka tu,wapumbafu, walio maadhuraau ‘watu maalum’ halafu,
inapigwa propagandakuwa ni IS, Al-Qaida auAl Shabaab. Kwa wale‘maadhura’, wanapelekeshwakufanya mambo wakidhaniawanafanya kwa akili zaona elimu zao, kumbewanaendeshwa kwa ‘remote’,akili zimeshikiliwa kutokambali.
Sasa wewe ukihangaika nahuyu ‘maadhura’, utakuwanawe maadhura vilevile.Ufumbuzi wa sawasawa nikumtafuta mpikaji wa fitna
hiyo, ukabiliane naye hatakwa kumzomea tu.
Ukisema kuwa waliofanyamauwaji Masjid Rahmanwalikuwa Waislamuwasiofuata Uislamu wa‘kizamani’, wa asili, ni sawana kutoa wito kwa wafiwa
na Waislamu kwa ujumlakuanza kuwasaka wafuasiwa huo Uislamu wa kisasa.Mkifika hapo, ni dhahirikwamba adui atatumiamwanya huo kuwahujumukupitia kundi moja huku yeyeakikaa pembeni. Ni hivyohivyo kama ikijengwa pichakwamba labda waliofanyauovu huo ni watu wa dininyingine katika wenzetuWatanzania. Na hilo ndiloanalotahadharisha AskofuDavid Mwasota.
Kwa upande wake Msemaj
wa Jeshi la Polisi KamishinaMsaidizi wa Polisi, AdveraBulimba amewatoa hofuwananchi kwa kuwahakikishikuwa nchi ipo salama.
“Kwa ujumla hali ya amanina usalama kwa nchi yetu nishwari …wananchi waondoehofu wakati Jeshi la Polisilikiendelea na uchunguzizaidi.”
Kamanda Bulimba alitoamaelezo hayo alipotakiwamaoni yake na gazeti la
Jibu la Maisha juu ya madaiya uwapo wa mitandaoya kigaidi ya kimataifa yaISIS na Al-qaida na tuhumakwamba mitandao hiyo ndiyoiliyohusika na mauwaji yaMasjid Rahman.
Ambalo tuna uhakikanalo ni kuwa haiwezekanikuwa na kundi lolote liitwela kiharamia au kigaidi,liwe la ndani au kutoka nje,ambalo linaweza kuweponchini, likaepuka macho yavyombo vyetu vya usalama.Na ambalo tuna uhakika nalopia, ni kuwa zile picha na
taarifa za kuwepo magaidiwa IS katika mapango yaAmboni, ni porojo, urongomtupu, mambo ya kuzua.Na ndio maana Kamandawetu Advera Bulimba, hanawasiwasi. Anasema, wananchwaondoe hofu, hali ya amanina usalama kwa nchi yetu nishwari kabisa. Kwamba, hayoyanayoelezwa na baadhi yawatu wasio tutakia mema, nipropaganda za kupandikizakitisho bandia ili maaduiwapate kufanya yao. (Somazaidi uchambuzi uk. 6 na 10)
KATIBU Mkuu wa Umoja wa Makanisa ya Pentekoste Tanzania(CPCT), Askofu David Mwasota.
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
4/20
4 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 201Tahariri/RATIBA
AN-NUUR S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786
Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM.www.annuurpapers.co. E-mail: [email protected]
Ofisi zetu zipo: Manzese Tip TopUsangi House, barabara ya Morogoro, D'Salaam
TUNACHUKUAfursa hii kukumbushaWaislamu kwa ufupikuhusiana na kupotezamaadili (kupoteamwelekeo tulioachiwana Mtume (s.a.w.) kamaalivyoamrishwa na Allah(s.w.) atufikishie. Nayeye amefufikishia.
Ni dhahiri kwambaWaislamu wameupotezaule Uislamutuliofundishwa na Mtume(s.a.w.) iwe ni kwa kujuaau kwa kutokujua.
Waislamu hawanaumoja, wamejigawamakundi kwa makundina kujengeana uadui waokwa wao, hali yakuwawameisahau kauli yaAllah (s.w.):
“Na shikamanenikatika kamba ya Allah(s.w.) wala msiachane.”(Qur. 3:103).
Kwa mtazamo wa
mafundisho ya Qur’an,kujigawa makundihakutaiepuka adhabu(kwa Allah (s.w.) kamaalivyosema Allah (s.w.).
"Tumeiteremshaadhabu kwa walewaliojigawa makundi".(Qur. 15:90).
Hatudhani kuwa jamiiya Waislamu hususanviongozi wa taasisi namashirika mbalimbali yaWaislamu hawajui ayahazi na makusudio yake.Lakini matokeo ya kibri, jeuri, hasad na tamaazimewafikisha Waislamuhapa walipo.
Tujiulize katika maishaya Mtume (s.a.w.)yalikuwepo makundikama haya tuliyojiundiasisi? Kama yalikuwepo, juhudi gani zilifanyikakuyamaliza na Waislamuwakabaki kitu kimoja?
Tunaona katikamazingira tuliyo nayosasa, ni dhahiri kwambatumepoteza mwelekeowa Uislamu na maadiliyake, sheria na Tawhiid,na kukubali kuchezewakama mwanasesere(toy) na makafiri kupitia
Tuache kibri tujengeumoja kwa Waislamu
udhaifu huu.Amewahi kusema
Mtume (s.a.w.),"Atakayeishi muda mrefu(Maswahaba) ataonamambo mengi ya uzushina jiepusheni nayo."
Kauli hii ya Mtume(s.a.w.) imetimia maanaumma wa Kiislamu
umetopea katikauovu na uzushi kamatunavyoshuhudiaWaislamu wakijigawakatika makundi nakujengeana uhasama nakupoteza umoja wao waKiislamu.
Huu si Uislamualiotuletea Allah (s.w.)kupitia kwa Mjumbewake. Tunajiuliza,kwa jinsi hali ilivyohapa nchini, ni naniataunusuru Uislamu (dinihii ya Mwenyezi Mungu)kama inavyosemaQur’an:
"Ni naniatakayeinusuru dini hii".(Qur. 61:14).
Wako wapi wanazuoniwa Kiislamu, viongoziwa Kiislamu, Masheikh,Maulamaa, Maimam,ambao kimsingi ndiodira katika kusimamiamiongozo ya dini, ndiowanaotegemewa kujengaumoja wa jamii yaKiislamu nchini.
Tukumbuke kuwaUislamu ni dhamanatuliyopewa na Muumbana kuamuru watu waishikatika ustaarabu wake.Ameeleza Mwenyezi
Mungu: "TumekuridhieniUislamu kuwa diniyenu." (Qur. 5:3).
Ni vipi tumeuachaustaarabu wa Uislamuambao Allah (s.w.)ameturidhia, kiasi chakubaki katika Uislamuwa vipande vipande haliya kuwa viongozi wapo?
Umoja katika Uislamuhapa nchini umepigiwakelele sana. Zimeelezwaathari walizopatana wanazoendeleakupata Waislamu kwakuwekwa kwao katika
mafungu mafungu, tenayanayohasimiana.
Lakini pamoja nakudhihiri athari nakufahamika kiini chatatizo, bado hadi sasahakuna hatua zozote zauhakika zilizochukuliwakunusuru hali.
Tunaona wakatiumefika wa hatua zamakusudi na za harakakuchukuliwa. BARAZAKUU, BAKWATA,MABARAZA yaWANAZUONI na Taasisinyingine za Kiislamunchini, pamoja na tofautizao za kifalsafa. Kunahaja ya kuketi na kuwekamkakati wa pamoja wa
kutengeneza jamii mojaya Waislamu nchini.
Tukiacha kibri na jeuri,tamaa za maslahi binafsi,chuki na husda, hililitawezekana na utakuwamwanzo mzuri kuitimizaaya ya Qur’an:
“Na shikamaneni
katika kamba ya Allah(s.w.) wala msiachane.(Msifarikiane).” (Qur.3:103).
Kama ni tofauti zenuza kifalsafa katikataasisi zenu, bakininazo, vumilianeni naheshimianeni kwazo,lakini hakuna haja yatofauti zenu hizo ziwesababu ya kuendelea
kuwagawa Waislamu.Ikiwa mtabaini
mapema na kutahayarina kuchukua hatua,mtaunusuru Uislamukwa kuweka kipaumbelecha umoja wao kwanza,maslahi ya taasisi baada
Tunaamini ikikosekan
jamii ya Kiislamuiliyojengwa katikamisingi madhubuti yaumoja, hakuna taasisimadhubuti ya Kiislamuitakayoweza kufaulukatika malengo yakekama ilivyokusudiwa.
Kama taasisi zenu nikwa ajili ya Waislamu, basi ni vyema mkajengaudugu wao kwanza.
1
1. “Enyi Mlioamini! Mmelazimishwa kufunga (Saumu) kama walivyolazimishwa waliokuwa kabla
yenu ili mpate kumcha Mungu.” Qur’an 2:1832. “ Na (huku) kufunga ni bora kwenu. Ikiwa mnajua.” Qur’an 2:1843. “Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi (atimize) hisabu (ya siku alizowacha kufunga)
katika siku nyengine Mwenyezi Mungu anakutakieni yaliyo mepesi wala hakutakieni yaliyomazito. Qur’auran.” Qur’an 2:185.
4. Vile vile Bwana Mtume (S.A.W) kasema: Kila kitu kina Zakka, na Zakka ya mwili ni Saumu.5. Anaefunga Ramadhani kwa Imani na kuzingatia (basi) hufutiwa madhambi yake yote
yaliotangulia. Na kama mngelijua faida iliomo k atika Ramadhani, basi mngetamani Ramadhaniiwe mwaka mzima.
J
RAMADHA N
YA :
MWEZI TAREHE
SIKU MUDA
WA
MWISHO
KULA
DAKU
(IMSAK)
KUINGIA
ALFAJIRI
ADHANA
KUCHWA JUA
JIONI
ADHANA YA
MAGHARIBI
KUFUNGUA
(IFTAR)
1 June 7 Ijumaane 11:00 11:15 12:15 12:20
2 June 8 Ijumatano 11:00 11:15 12:15 12:20
3 June 9 Alkhamisi 11:00 11:15 12:15 12:20
4 June 10 Ijumaa 11:00 11:15 12:15 12:20
5 June
11 Ijumamosi 11:00
11:15
12:15
12:20 6 June 12 Ijumapili 11:01 11:16 12:16 12:21
7 June 13 Ijumatatu 11:01 11:16 12:16 12:21
8 June 14 Ijumaane 11:01 11:16 12:16 12:21
9 June 15 Ijumatano 11:01 11:16 12:16 12:21
10 June 16 Alkhamisi 11:01 11:16 12:16 12:21
11 June 17 Ijumaa 11:01 11:16 12:16 12:21
12 June 18 Ijumamosi 11:02 11:17 12:17 12:22
13 June 19 Ijumapili 11:02 11:17 12:17 12:22
14 June 20 Ijumatatu 11:02 11:17 12:17 12:22
15 June 21 Ijumaane 11:02 11:17 12:17 12:22
16 June 22 Ijumatano 11:02 11:17 12:18 12:23
17 June 23 Alkhamisi 11:03 11:18 12:18 12:23
18 June 24 Ijumaa 11:03 11:18 12:18 12:23
19 June 25 Ijumamosi 11:03 11:18 12:18 12:23
20 June 26 Ijumapili 11:03 11:18 12:18 12:23
21 June 27 Ijumatatu 11:04 11:19 12:19 12:24
22 June 28 Ijumaane 11:04 11:19 12:19 12:24
23 June 29 Ijumatano 11:04 11:19 12:19 12:24
24 June 30 Alkhamisi 11:04 11:19 12:19 12:24
25 July 1 Ijumaa 11:04 11:19 12:19 12:24
26 July 2 Ijumamosi 11:04 11:19 12:19 12:24
27July
3Ijumapili
11:05 11:20 12:20 12:25
28 July
4 Ijumatatu 11:05
11:20
12:20
12:25
29 July 5 Ijumaane 11:05 11:20 12:20 12:25
30 July 6 Ijumatano 11:05 11:20 12:20 12:25
DUA YA KUSOMA UNAPOFUNGUA
“ALLAHUMA LAKA SUMTU WAALA RIZKIKA AFTARTU”
DUA YA KUSOMA UNAPOFUNGUA
“ALLAHUMA LAKA SUMTU WAALA RIZKIKA AFTARTU”
KALENDA YA RAMADHANI
Mwaka 2016
KALENDA YA RAMADHANI
Mwaka 1437H
RAMADHANI KARI M
ALLAH UMMA
I NNAKAAF UWW UNT UHI BB U-L-AF
UA
FAA
F UANNAYAKA RI MAL-AF UA
Nyakati hizi za muda wa kuftari namwisho wa daku, zimezingatia mazingiraya Zanzibar. Katika miji mingine, kutakuwana kuongezeka dakika za ziada kulinganana muda wa kutoka na kuzama jua katikaeneo husika.
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
5/20
5 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 201Habari za Kimataifa
baada ya kundi hilo la Waislamukukilinganisha chama chake nautawala wa Manazi.
Baada ya kuvunjika
kwa mkutano huo Rais waBaraza Kuu la Waislamunchini Ujerumani AimanMazyek, alisema chama chaAfd kimethibitisha kwambakinakusudia kuendelea nasera yake kali ya mrengowa kulia,kuchafuwa sifa yaWaislamu na kupalilia chukiisiokuwa na msingi.
Aiman Mazyek, Kiongozi waBaraza Kuu la Waislamu nchiniUjerumani (ZMD), ambayendiye aliyefanya juhudi zakufanyika kwa mkutano huokatika hoteli moja mjini Berlin,alisema msimamo wa chamahicho cha AfD dhidi ya Uislamuunakiuka katiba kwasababuunaibaguwa dini nzima yaKiislamu.
"Tunasema kwamba katibasio suala la mjadala kwetu.Na huo ndio msingi wamazungumzo yetu. Nasikitikakusema kwamba chama chaAfD kimejitoa katika mkutano bila ya kutimiliza malengo yake.Na hakuna yoyote kati yaoaliyekuwa tayari kuzungumziamasuala makuu katika sera yao.Miongoni mwao ni madai yanamna ya kujenga misikiti yetu,mabucha ya nyama za halali nakadhalika.“ alifafanua kiongozihuyo.
Mazyek ambaye kundi lake
linawakilisha sehemu tu ya jami ya Waislamu milioni nnenchini Ujerumani, alisema hukonyuma kwamba chama cha
AfD wapiga kampeni kuzuia ujenzi wa Misikit
AfD ni chama cha kwanza chaUjerumani tokea utawala wa
Hitler ulipoidunisha na kutishiakundi zima la kidini.
Mazyek hakutengua kauliyake ya kukilinganishachama hicho na utawaka waManazi baada ya kuvunjikakwa mkutano huo, akisisitizakwamba sera ya AfDinamkumbusha zama zakiza kabisa katika historia yaUjerumani.
Awali kulikuwa na mvutanomkubwa kutoka pande zotembili kabla ya kuanza kwamkutano huo na penginekutokana na kujua mazingira yakisiasa yanayokizunguka chamahicho, ambapo kilituma ujumbe
mchanganyiko kwenye vyombovya habari na Mwenyekitimwenza wa chama hicho JörgMeuthen, yeye alisema Misikiti
ni sehemu ya Ujerumani namahala pa kufanya ibada hivyoinabidi tu, waangalie kwamakini nini kinachohubiriwahapo.
Lakini mwenzake FraukePetry, alikuwa na kauli kalikwa kusema kwamba iwapozaidi ya nusu ya Waislamuwanazipa umihumu zaidi sheriza Kiislamu "sharia" kulikosheria za taifa jambo hilo litakujkushindwa kudhibitiwa.
Mwanamama huyoakilalamika kufuatia kuvunjikakwa mkutano huo, kwambaupande wa pili umekataakuzungumzia juu ya masualamahsusi kama vile sheria za
Kiislamu na kudai chamahicho kikanushe sera yakeambayo imesema ilipitishwakidemokrasia.
Rais wa Baraza Kuu la Waislamu nchini Ujerumani Aiman Mazyeakisalimiana na Mwenyekiti Mwenza wa chama cha AfD FraukePetry mjini Berlin. Parstoday/DW.
CHAMA chenye msimamomkali cha mrengo wakulia Ujerumani cha TheAltenative for Germany (AfD)
kimependekeza kusitishwaujenzi wa Misikiti nchinihumo. Tayari Chama hichokimeitisha maandamano yakupinga ujenzi wa Msikiti huo.
Chama hicho ambacho ni chatatu kwa umashuhuri nchinihumo, hivi karibuni kilibainishawazi kuwa kitapinga ujenzi waMsikiti wa kwanza katika jimbola Thuringia, Mashariki mwanchi hiyo.
Kiongozi wa chama hicho,Bjorn Hocke, alidai kuwa ujenziwa Misikiti katika jimbo hilo nisehemu ya mpango wa mudamrefu wa Waislamu kuenezaushawishi wao.
Msimamo wa chama hichoumeibua wasiwasi kuhusukuibuka upya vyama vyamrengo wa kulia vyenyemisimamo mikali ambavyovinalenga kuibua malumbano naWaislamu takriban milioni nnenchini Ujerumani.
Hivi karibuni chama hichokilizindua kampeni ya kusema‘Uislamu si sehemnu yaUjerumani”.
Chuo Kikuu cha Kiislamucha Azhar kupitia taasisiyake ya kukabiliana na chukidhidi ya Uislamu, kimeshatoataarifa na wito kwa taasisi zaKiislamu nchini Ujerumanikutumia uwezo wao wa
kisheria kukabiliana na chukizinazoenezwa na AfD.
AfD pia kinapinga seraya serikali ya nchi hiyo yakuwakaribisha wakimbizi,kilitoa pigo kwa chama chaChancelor Angela Merkel, katikauchaguzi wa majimbo Machimwaka huu.
Waislamu katika nchiza Magharibi wamekuwawakikabiliwa na wimbi jipyala chuki dhidi ya Uislamu(Islamophobia) hata baada yakuwa wamelaani vikali hujumaya kigaidi duniani na hasazilizotokea katika miji ya Parisna Brussels.
Wakati chama hichokikiazimia kuzuia kujengwaMisikiti Ujerumani, ule mkutanouliokuwa ukisubiriwa kwahamu kati ya AfD na Kundila Kiislamu umemalizika kwamabishano makali Jumatatu wikihii na kuvunjika nusu saa tu baada ya kuanza, huku kiongoziwa kundi hilo la Kiislamuakisema kuwa chama hicho chasera kali za mrengo wa kuliandicho kilichoamuwa kuuvunjamkutano huo.
Mwenyekiti mwenza wa AfDFrauke Petry, alisema hakunakilichobakia kuzungumzia
KASISI Ma’auga Motu,ambaye ni Katibu Mkuu waBaraza la Makanisa ya Samoa,ameishinikiza serikali yavisiwa hivyo kupiga marufukuUislamu katika visiwa hivyo.
Tayari Waziri Mkuu wanchi hiyo, Tuilaepa SaileleMalielegaoi, wiki iliyopita alitoawito wa kufanyiwa marekebishovipengele vya uhuru wakuabudu katika katiba ya Samoa.
Waziri huyo alisema agizolake linalenga kuhakikishaitikadi za Kikristo zinaingizwakikamilifu katika katiba hiyo.
Kwa msingi huo, KasisiMotu amemtaka Waziri Mkuuhuyo kusonga mbele zaidina jitihada zake za kuupigamarufuku Uislamu nchini humo,ambao amedai ni tishio kwamustakabali wa nchi hiyo.
Kasisi huyo amebainishawasiwasi wake kuhusukuongezeka idadi ya watu
Samoa mbioni kupiga marufuku Uislamuwanaovutiwa na Uislamu nchinihumo na hivyo kuwafanyaWaislamu wawe na ushawishi.
Kufuatia matamshi hayo yachuki na hatari dhidi ya Uislamuvisiwani humo, Imamu Mkuuwa Samoa amesema Wakristokatika kisiwa hicho wanapaswakuvumilia dini nyingine nakuacha vitendo vya kibaguzi.
Imam Dkt. Mohammad binYahya, aliashiria kuwa iwaposerikali ya Samoa itazingatiamakusudio yake, basi kunauwezekano mkubwa wa serikalihiyo kupata matatizo makubwaya kufanya biashara na nchi zaKiislamu iwapo katiba ya nchihiyo itabadilishwa.
Katika sensa ya mwaka 2001,ilibainika kuwa asilimia 0.03 yawakazi wote wa visiwa hivyoni Waislam, huku walio wengiwakiwa ni Wakristo.
Samoa ni nchi ya visiwailiyopo katika Bahari ya Pasific
inayojumuisha visiwa viwilivikuu vya Savai’i na Upolu navisiwa vingine vidogovidogo.Ni nchi iliyo kati ya Hawai’i naNew Zealand, mji wake mkuuukiitwa Apia huku idadi yawatu wake ikikadiriwa kuwa ni190,000. Parstoday.
Imam Dkt. Mohammad bin Yahy
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
6/20
6 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 201Makala
WAKATI safari yaRais Barack Obama waMarekani nchini SaudiArabia mwezi Aprili 2016ikiwa inaiva, Bunge laMarekani lilianza mjadalawa sheria kuhusu dola(nchi za nje) zinazowezeshaugaidi (JASTA) ambayopamoja na mambomengine ingewezeshafamilia za walioathirikana mashambulio yaSeptemba 11 kuishitakiserikali ya Saudi Arabiakwa uharibifu. Pia mweziAprili 2016 gazeti la NewYork Times lilichapishataarifa kuwa uchunguziwa kamati ya Bunge nchiniMarekani mwaka 2002kuhusiana na mashambulio
ya Septemba 11 ilifikiatamati kuwa maofisa waSaudia waliokuwa wanaishiMarekani wakati huo,walikuwa na mkono katikanjama hizo. Hitimisho hilola tume, gazeti hilo lilisema,liliainishwa katika taarifaambayo bado haijatolewahadharani.
Muswada wa JASTA,ambao ulipitishwa na Barazala Seneti May 17, 2016ulizua tafrani huko Saudia,ikijionyesha katika taarifaya Waziri wa Mambo ya Njewa Saudia na mashambulizi
makali dhidi ya Marekanikatika vyombo vya habari vyaSaudia. Aprili 28, 2016, gazetila Saudia linalochapishwaLondon, Uingereza la AlHayat lilichapisha makalakali sana kuhusu suala hiloiliyoandikwa na mtaalamuwa sheria wa Saudia KatibAl-Shammari, ambaye alitoahoja kuwa Marekani yenyeweilipanga na kutekelezamashambulizi ya 9/11, hukuikielekeza lawama zake kwawengine ambao wamekuwawanabadilikabadilika.Kwanza ilikuwa ni Al Qaeda
na Taliban, halafu utawala waSaddam Hussein nchini Irak,na sasa Saudia. Alisema kuwavitisho vya Marekani vyakufichua ripoti za uchunguziambazo inadai zinaonyeshakuhusika kwa Saudia katikamashambulio, ni sehemuya mbinu za kawaida zaMarekani kufichua taarifaza washindani ili kuwapiku,ishinde. Ilisema mbinu hiyoinaitwa “ushindi kwa kutumianyaraka zilizohifadhiwa”(victory by means of archives.)
Yafuatuo ni maelezo
Dola zinazowezesha ugaidiMarekani ilipanga mashambulio ya Sep. 11 2001Lakini inasakama nchi nyingine kwa matukio hayo
Na MEMRI - Taasisi ya utafitihabari ya Mashariki ya Kati
kutoka katika makala ya Al-Shammari:
“Wale wanaofuatilia seraza Marekani wanaona kuwazimejengwa katika msingiwa kupanga mapema nakuangalia yanayowezakutokea baadaye. Hii ni kwasababu mara nyingine inatoasuala kwa nchi fulani ambayoMarekani haitaki (kuliwekawazi) kwa wakati huo, ilainalihifadhi kama turufukwa wakati ujao ili kutoashinikizo kwa nchi hiyo.
Yeyote anayeangalia upya(taarifa za aliyekuwa Rais waMarekani) George HerbertW. Bush kuhusu ‘OperationDesert Storm’ (kuing’oa Irakkutoka Kuwait mapemamwaka 1991) anawezakugundia kuwa Bush anakirikuwa Jeshi la Marekanilingeweza kuwa limevamiaIrak katika miaka ya 1980,lakini Marekani ikaona kuwaimwache Saddam Hussein iliawe nyenzo katika mivutanokati ya Marekani na nchi zaGhuba. Hata hivyo, wakatiwimbi la u-Shia lilipoanza
kusonga mbele, Wamarekaniwalitaka kumwondoaSaddam Hussein kwanihawakuwa wanamwona tenakama turufu mikononi mwao.
“Septemba 11 ni moja yaturufu ambazo Marekaniinazo kwenye hifadhi zakekwani watu wote wenye
busara duniani wanaoihakikisera ya nje ya Marekani nawanaochambua picha zavideo kuhusu Septemba11, wanakubali kwa sautimoja kuwa kilichotokeakatika Minara Pacha (Twin
Towers-WTC) ilikuwa nikitendo cha Marekaniyenyewe, kilichopangwana kutekelezwa ndani yaMarekani. Uthibitisho wasuala hili ni mfululizo wamilipuko ambayo ilichanamajengo yote mawili.
Wataalamu wa uhandisimifumo waliyaangusha kwamilipuko, wakati ndegezilizobamiza katika majengohayo zilitoa tu mwanga (wakijani) wa kuendelea na zoezila kulipua, na ndege hizo
hazikuwa sababu ya majengohayo kuanguka. Lakini badoMarekani inaelekeza lawamazake pande zote. Sera hiiinaweza kuitwa ‘ushindi kwakutumia hifadhi nyaraka.’
“Mnamo Septemba 112001 Marekani ilifikiaushindi katika maeneokadhaa kwa wakati mmoja,ambako hata wahafidhina(wapenda vita) waliokuwepowakati huo Ikulu yaMarekani, wasingewezakutazamia. Sababu zinawezakuorodheshwa kama:
“1. Marekani iliunda,
katika hisia za watu, aduiasiyeonekana - ugaidi- ambao umekuwa kileambacho marais wa Marekaniwanakilaumu kwa makosayao yote, na pia kimekuwasababu pekee ya opereshenizozote chafu ambazowanasiasa nchini Marekanina maofisa wa kijeshiwanataka kufanya katika nchiyoyote ile. Nembo ya ugaidiikapachikwa Waislamu, nahasa Saudia.
“2. Ikitumia tukio hilo,Marekani ilianzisha wimbi
jipya la ukusanyaji wa silahaduniani. Kila mmoja akahitajkupata silaha za kila ainakujilinda wenyewe na wakatihuo huo kupambana naadui asiyeonekana, ugaidi- licha ya kuwa hadi sasahatufahamu nini hasa hikiambacho Marekani inaita
ugaidi, ila tu kusema kuwa nwa Kiislamu.
“3. Marekani iliwafanyawananchi wake kuchagua kaya vitu viwili vibovu: Waishikwa amani lakini wawekatika hatari ya kufikia kifo(kutokana na ugaidi) au wafenjaa huku wako salama kwan
bajeti ya nchi hiyo itatumikakuwapeleka wanamaji waMarekani hata kwenda sayarya Mars kuwalinda wananchwa Marekani.
“Tazama, leo tunaonanyaraka hizi zilizohifadhiwazinatolewa mbele yetu:Mahakama ya jiji la NewYork inadai kuwa Iraninahusika na shambulio laSeptemba 11, na pia tunaonamuswada wa sheria Bungela Marekani unaodai kuwaSaudia ndiyo inayohusikana tukio hilo. Hii ni baadaya utawala wa awali waIrak kushukiwa au kutajwakuwa ulihusika. Al Qaedana Taliban walilaumiwapia kuwa walihusika, nahatujui nani atakayedaiwahapo kesho kuwa anahusika!Lakini, (hata awe nani)
hatutashangaa hata kidogokwani huu ndiyo mpangiliowa utumiaji wa nyarakazilizohifadhiwa Marekani,kuwa ndivyo ustaarabu,kuheshimu uhuru wa mtu
binafsi na demokrasia. ni jinsinavyofanya kazi.
“Kiini cha hulka yaMarekani ni kuwa haiwezikuishi bila adui. (Kwa mfano
baada ya muda ambakohaijapigana na nchi yoyote(yaani, baada ya Vita Vikuuvya Pili), Marekani iliundaaina mpya ya vita, vita baridivya kiitikadi. Halafu, enzi
za Urusi ya kikomunistizilizokwisha, baada ya sisiWaislamu kuwasaidia wenyedini kupigana na ukomunistikwa ajili ya (kuisaidia)Marekani, wakaanza kuonaWaislamu kama ndiyo aduiyao mpya! Marekani ilionaulazima wa kuunda aduimpya - ikapanga, ikajikusanyna kutekeleza dhamira hiyo(ili kuwalaumu Waislamukwa ugaidi). Hii haitamalizikhadi Marekani ifikie malengoambayo imejiwekea yenyewe
Inaendelea Uk.
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
7/20
7 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 201Kalamu ya Ghassani
Na Mohammed Ghassani
WANANCHI wakiwania kumpa mkono Maalim Seif Sharif Hamad,siku ya Ijumaa ya tarehe 27 Julai 2010, Fuoni Zanzibar.
Picha awiri makala hiiniliipiga tarehe 24 Julai2010, nje ya msikiti waIjtimai, Fuoni, magharibi yakisiwa cha Unguja. Angaliahuyo mtoto mkono wakushoto ambaye anawaniakumpa mkono Maalim
Seif Sharif Hamad. Nakisiakuwa wakati huo alikuwana miaka 12 au 13, umriambao anao mtoto wanguwa kwanza hivi sasa. Kwahivyo, sasa ana miaka 18au 19 na yumkini alikuwampiga kura kwenyeuchaguzi wa Oktoba 25.Naamini alimpigia kuraMaalim Seif.
Wakati napiga picha yamvulana huyu akiwaniakumpa mkono Maalim Seifsiku hiyo, kumbukumbu ya
siku ya kwanza kumuonakiongozi huyu uso kwamacho ilinirejea kichwanimwangu. Nakumbuka,nikiwa na umri wa miaka7 au 8, Maalim Seifalikuwa Waziri Kiongoziwa Zanzibar na alikujakutembelea Kambi ya Jeshila Kujenga Uchumi (JKU)Msaani, wakati huo bondela Msaani lilikuwa kwenyempango wa MTAKULAaliouanzisha yeye kwa ajiliya kuitosheleza Zanzibarkwa chakula.
Baada ya ziara yake,akaamua kukutana nawananchi wanaoishipembezoni mwa bonde hilona kambi yenyewe ya JKU,awasikilize malalamikoau maoni yao. Mmoja waoalikuwa baba yangu (Allahamrehemu), ambaye wakatihuo alikuwa anakaribiaau amepindukia kidogomiaka 60. Malalamiko yakeyalikuwa ni juu ya sehemuya shamba letu la MtiMkuu ambalo lilichukuliwa
Baada ya kukosa Urais…
Maalim anaelekea wapi?Hata hivyo, alikuwa na daima atakayekuwa
na uongozi wa JKU bila yaridhaa yake na tena likiwahalihusiki kabisa na bondela Msaani unakolimwampunga wa mradi waMTAKULA.
Nadhani chiniya mpango huu waMTAKULA serikaliilikuwa imewaruhusu JKU
kuchukuwa ardhi yoyoteambayo wanaona inafaa baada ya makubaliano nawenye ardhi hiyo. Lakiniyetu sisi ilikuwa upande wa juu na sio bondeni, hivyohaikufaa kulimwa mpungawa umwagiliaji. Mkutanoulifanyika kwenye bandala JKU na baba akasimamakuelezea malalamiko yake.
Wakati huo, badokiwango cha woga wawananchi kwa serikalikilikuwa kikubwa nailitaka ujasiri kwa mzee wa
kijijini kusimama mbele yaumma kulisema Jeshi hilokwa ubaya. Maalim Seifakamuuliza baba yangu:
“Je, umeshapelekamalalamiko yako haya kwangazi husika?”
Baba akamuambiaalishapeleka, na ameshafikahadi kwa mkuu wamkoa wa KaskaziniPemba wa wakati huo,Maalim Masoud OmarSaid (Allah amrehemu),ambaye alikuwepo kwenye
mkutano huo, akiwa mezakuu.
Huyu Maalim Masoudalikuwa pia mtu waPandani, yeye akitokea KwaMwewe kwa Mabatawi, sisiwa Mchangani. Alikuwakatika wasomi wa kwanzawa Pandani, nadhani alifikaMakerere. Baadaye, kamailivyokuwa kwa mkuu wamkoa wa kusini Pemba,Maalim Juma Ngwali(Allah amrehemu), alikujaakawa muasisi wa CUF.
Maalim Seifalipomgeukia MaalimMasoud kumuuliza,Maalim Masoud akamruka baba yangu. “Hapana,Bwa’ Khelef hujawahi kujana suala hili!” Baba yanguakainuka kama katiwamoto, tena kwa hasira:“Bwan’ Masoud, watakanije hapo tusutane?”
Akawa anatia mkonomfukoni kutoa barua zaMkuu wa JKU, Mkuu waWilaya, Chameni Mzee Juma Mansour na yakeyeye mkuu wa mkoa. Babaalikuwa na tabia, ambayoamenirithisha mimi, yakuweka kumbukumbu yamaandishi ya takribanikila kitu. Mwenyewealijifundisha kusoma,kuandika na kuhesabukwa hati za Kizungu akiwamtu mzima, lakini alikuwa
anajuwa kuyafanya yotekwa uhodari mkubwa.
Maalim Seif akajuwakuwa hapa aibu itazuka.“Basi mzee. Suala lakolitashughulikiwa maramoja.” Siku hiyo, nilitokanjia nzima nimemshika
mkono baba yangunikijirusha huku na kulekwa furaha. Nadhanimoyoni nilikuwa najioneafakhari kuwa baba yanguamesimama mbele yaserikali yote na akasemakwa ushujaa. Hadithi zotezilikuwa kuhusu yeye sikuhiyo.
Maalim Masoud alikujakumtembelea baba dukanikwetu siku chache baadayeNakumbuka alikuwaanaendesha gari ya LandRover rangi ya chai ya
maziwa. Mazungumzo yaosikuyasikia, lakini baadaya kiasi cha mwezi hivi,tukarejeshewa shamba letuShamba lenyewe si kubwa,lakini lilitosha kutupawasaa wa kulima muhogona viazi na kupandaminazi, ambayo masikini baba yangu hakuwahikuishi akaja akaona ikizaa.
Picha nzima ya mkasawenyewe imesalia hadileo kichwani mwangukama mkanda wa vidio.
Nakumbuka mvua,matope, utelezi wa mlimawa Kombo Hawana, sareza kijani za JKU, mpungauliowanda kwenyechanjaa la Msaani, surayake Maalim Seif, kanzualiyovaa baba na kofiayake ya kudengua, suraza watoto wenzanguwaliokuwepo na yote.
Hiyo ilikuwa mara yanguya kwanza kumuonaMaalim Seif uso kwamacho. Huyu ndiye MaalimSeif alivyojiwasilisha
kwangu nikiwa mtotowa miaka 7, na hiyondiyo kumbukumbualiyoniwacha nayo hadi leonikiwa nakaribia miaka 40.Mtu wa haki wa zama zote Jana, leo na kesho.
Siku nyengine nitakujakusimulia namna ambavyomwaka mmoja baadayenilikuja kumuambiakuwa “nataka kuwa kamaMaalim”, naye akaniambia“kuwa”, lakini bahatimbaya sikuwa.
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
8/20
8 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 201Makala
Dola zinazowezesha ugaidiInatoka Uk. 6
“Sasa kwanini mafanikiohaya yasielekezwe kwautawala wa Marekani, wakatimakampuni ya bima yanalipiauharibifu huo, iwe ni ya ndaniau nje? Hii, ndugu zanguWaarabu na Waislamu, ndiyo
sera ya kuhifadhi nyaraka yaMarekani.”
Udanganyifu wa habari:Saudia kudaiwa kuishambuliaMarekani
Na Paul Craig Roberts
May 27, 2016 - Mtandao waKupashana Habari
Maelezo kuhusumashambulio ya Septemba11 2001 yanayobadilika kila
siku, yameingia katika hatuampya. Lawama zinaelekezwakutoka kwa Osama bin Ladenkwenda kwa serikali ya SaudiArabia.
Kuna kurasa 28 za sirikatika taarifa ya uchunguziya Bunge la Marekanikuhusu mashambulizi ya9/11 ambazo ziliyakinishamisaada ya kifedha ya Saudiakwa wateka nyara wa ndegezilizobamiza majengo pachakatika mashambulizi hayo.Si utawala wa George W.Bush au Obama ambao
ulikuwa tayari kuchapishakurasa hizo. Ni wajumbewachache tu wa mabaraza yakutunga sheria ya Marekaniwameruhusiwa kuzisoma, nahawaruhusiwi kuzungumziawalichosoma.
Hata hivyo, Bunge laMarekani sasa limepelekewamuswada kuhusu ‘Sheriaya Kushitakiwa kwaWafadhili wa Ugaidi’ ambayoikipitishwa, inawezeshafamilia za walioathirikana mashambilizi ya 9/11
kuishitaki serikali ya Saudiakulipwa fidia. Kwa manenomengine, licha ya kuwaBunge la Marekani halinahabari isipokuwa vianziovya kudakiza vinavyoungamkono muswada huo,wajumbe wa mabaraza hayowanaendelea na mchakatowa sheria hiyo, na Obamaanasema wakiipitisha, yeyeatakataa kuitia saini. Kukataakutoa hadharani ushahididhidi ya Saudia na tishio lakutumia mamlaka ya kukataa
kutia saini kumefanya
wachambuzi wengikushabikia suala hilo.Ni kitu gani kinaendelea
hapo?
Jibu mojawapo ni kuwakukubalika kwa maelezo yaserikali kuhusu kilichotokeakatika mashambulizi yaSeptemba 11 kunapunguakutokana na maelezo hayokushambuliwa na wataalamumaeneo mengi. Ili kuelekezaupya hisia za wananchi,linazushwa jambo jipya katikamchakato mzima wa suala
hilo. Tuhuma kuhusu Saudiazinayakinisha kuwa kuna ainafulani ya uficho wa serikalikuhusu tulio hilo lakini inatoatuhuma hizo kutoka Marekanikwenda Saudia. KuituhumuSaudia pia kunakidhi hajaya wahafidhina waliokuwamadarakani wakati huokupindua serikali za Saudia,pamoja na serikali za Irak,Syria na Iran. Kama wananchiwa Marekani wanawezawakainuliwa hamasa dhidiya wa-Saudi, wahafidhina
wanaweza kufikia malengoyao ya kubadili utawalanchini Saudia.
Inaelekea tunaingia katikahali ya udanganyifu wahabari kwa kina yenye niaya kulinda maelezo rasmipotofu kuhusu matukio ya9/11. Shauku na shaka yawananchi wa Marekani sasainaelekezwa kwa Saudia, nachuki ya raia wa Marekaniinaelekezwa kwa serikali yanchi hiyo kuficha uhusikawa Saudia katika tukio hilo.
JENGO la Pentagon, Marekani.
Sababu zinazofanya ripoti
hiyo isiwekwe hadharanimoja ni kuwa ni taarifaya kutungwa tu ambayoikitolewa hadharaniwataalamu watafichuaudhaifu wake. Kwa upandemwingine, inaweza kuwa nitaarifa potofu iliyotolewa kwatume ya uchunguzi (ya Bungela Marekani) na wahafidhinaambao walitumiamashambulizi hayo kuanzakuilenga Saudia ipigwe naMarekani.
Hakuna maelezoyaliyotolewa kwanini Saudia,ikiwa na uhusiano wa karibuna Marekani kwa miaka yotena hata ukaribu na familia yakina Bush (kwa mfano babawa Osama, Mohamed binLaden alifia Marekani kwaajali ya ndege binafsi akiwakatika shughuli za kibiasharana mapumziko kwa akinaBush, jimbo la Texas nchinihumo), iwe na haja yoyoteya kuwezesha shambulio lakigaidi dhidi ya Marekani.Utawala wa Saudia (kwa jadi)unahitaji ulinzi wa Marekani.
Hauna haja hata chembe yakufanya taifa linalotoa ulinzikwake lionekane kuwa dhaifuna kudhalilishwa na kikundikidogo cha vijana walioshikavisu vya kukatia makasha (navitungu jikoni). Dola dhaifukiasi hicho haiwezi kutoaulinzi wowote.
Isitoshe, Saudia inapiganavita Yemen kwa ajili yaMarekani. Kama wa-Saudia wanataka kuidhuruMarekani, kwanini isiiache
Marekani ipigane vita vyakeyenyewe nchini Yemen?
Ifuatayo ni hisia ya m-Saudkuhusu kuhusika kwa nchihiyo katika shambulio laSeptemba 11:
Katib Al-Shammarianasema kuwa Marekani
ilipanga na kutekelezashambulio la 9/11 ili kupatanguvu za kufanya maamuzimakubwa kuhusu Masharikiya Kati na ikaelekeza lawamakuhusu shambulio hilo kwanchi au watuhumiwa tofautikulingana na malengo yaMarekani katika nyakatitofauti. Kwanza ilikuwa niOsama bin Laden, Al Qaedana Taliban. Halafu SaddamHussein na Irak. Mahakamamoja ya New York iliilaumuIran. Sasa Saudia inapewanafasi ya kuwa muhusikawa tukio hilo. Wamarekanianasema, wakati wotewanakuja na nyaraka zenykutia shaka na kudai wanaushahidi ambao hata hivyohawautoi hadharani.
Wamarekaniwangefaidika sana kwakusoma wanachosemawengine. Tunasomamaelezo ya wa-Saudikuhusu matukio yaSeptemba 11? Yanaingiaakilini kuliko maelezorasmi yanayotolewa nchini
Marekani.(Dk. Paul Craig Robertsalikuwa Naibu Waziri wa Fedha mwenye dhamanaya sera za uchumi namhariri mshiriki wa gazetila kitaaluma la WallStreet Journal. Amekuwamwanasafu wa jarida laBusiness Week, mtandaowa habari wa Scripps Howard, na klabu yawaandishi wabunifu,Creators Syndicate. Amekuwa na vipinditofauti vya kufundishakatika vyuo vikuumbalimbali, na makalazake katika mtandao zinawafuasi kote duniani.vitabu vya hivi karibuni vyDk. Roberts ni ‘Kushindwakwa Ubepari wa Soko
Huria,’ na ‘Mparaganyikowa Uchumi katika nchi za
Magharibi,’ ‘Jinsi AmerikaIlivyopotezwa,’ na ‘Hatari yUhafidhina Mamboleo kwa
Amani Duniani.’)
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
9/20
9 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 201Tangazo
ni wakati wa kupeanatalaka ya muda. Dhanailiyopo ni kuwa kimadahawezi kukupikiafutari, itakuwa swaumuhaikubaliki.
Katika kundi hilowapo pia wale ambao,huvifanya vilabu vyapombe kupungukiwana wateja kwa muda nakwa upande mwingine,Misikiti kupata wageniwengi kwa wakatimmoja. Misikiti itafurikakatika kumi la mwanzo,sambamba na vilabu vya
Vunja Jungu
masaa yote na miaka yote. Halafulengo la kufunga ni ili tuwewachamungu. Yaani Ramadhaniinakuwa kama chuo cha mafunzo,
uwanja wa mazoezi, na mechi ndiomaisha ya kila siku.Unapofunga, inakuwa ni wewe
na Mungu wako. Unaweza kudaiumefunga lakini ukajifungia ndaniukala na kunywa, ukitoka njehakuna anayejua. Lakini hufanyihivyo kwa sababu unaamini kuwahata kama hakuna mtu anayekuona,Mungu anakuona. Sasa hofuhiyo na namna hiyo ya kutambuakuwa Mungu yupo na anakuonaukifanya jambo baya, uingize katikamatendo yako ya kila siku baada yaRamadhani.
Hatutakiwi tuingie katikaRamdhani na dhana potofu kuwa
Mungu yupo katika Ramadhanitu. Ndio unaona watu wanaletamambo ya vunja jungu. Kamahivi, wapo watakaozini mabinti
za watu wakisema ni vunja jungu,wanamaliza kiu kabla ya mwezi watoba. Unachotakiwa kufahamu nakuzingatia ni kuwa, yule Munguunayemwogopa na ukawa hulimchana wa Ramadhani mafichoni,kwa kujua kuwa anakuona, basiujue kuwa hata ukiwa gesti leo aumahali popote ukifanya uchafu wazinaa, basi ujue anakuona.
Halafu kwa wale wanaofanyauchafu wakidai kuvunja junguna kutarajia kutubia wakati wakufunga, je, wana mkataba gani naMungu kwamba hatawafisha kablaya Ramadhani. Wangapi tumesikiawamefia katika madanguro (guest
KWA baadhi ya watu,Ramadhani ni mweziwa biashara. InapofikaRajab, wenye madukaya nguo, ndio msimu wakwenda Dubai, China,Hong kong, Uturuki nasehemu kadhaa kuletabidhaa wakijua kuwa
Ramadhani msimu wabiashara. Watu watatakanguo za sikukuu yaEid el Fitri. Wenginewatahakikisha tambi zakila sampuli zipo, tende,mchele, maharage naunga wa ngano.
Kwa watu wa biasharaza vyakula sokoni,watahakikisha kuwamihogo, magimbi,ndizi, nazi na mbatata,hazikosekani. Huo kwaoni mwezi wa kuchuma.
Wapo pia ambaoRamadhani ni mweziwa laghawi. Mwezi wakucheza karata, drafti
na bao. Wanasemawanapoteza mudakusubiri muda wakuftari. Basi hao watakaakwenye bao masaakadhaa, swala zitawapitahapo hapo wala hawanahabari.
Wengine Ramadhani nimwezi wa Mungu. Kamawalikuwa na vimadawao, watawapa likizoya mwezi. Wenye kuishi bila ndoa, huo unakuwa
pombe (bar) kukosa wateja. Lakinikadiri siku zinavyoyoyoma nazile za Eid kukaribia, ndivyo watu
wanavyozidi kupungua na wale wa bar kuongezeka.Hapa unawakuta pia wale
ambao, huikaribisha Ramadhanikwa kufanya maasi sana, wenyewewanaita vunja jungu. Na huiagaRamadhani kwa mtindo huohuo. Eid badala ya kuwa sikuya kumshukuru Mungu nakumkumbuka kwa wingi, waondiyo siku ya kukamia kufanyamaasi waliyokuwa wameyaachakwa mwezi mzima.
Tunalopaswa kufahamu ni kuwaibada sio kwa mwezi mmoja tu.Mungu hayupo katika Ramadhanipekee. Mungu yupo siku zote,
houses) wakiwa nawapenzi wao. Hebufikiria unaingia leogesti na mke wamtu au binti wawatu halafu unafiahapo au yeye anafiakifuani kwako!!!”
Kwa bahati mbaykabisa, wengi wetu
tunachozingatiakatika kufunga,ni kuacha kula,kunywa, kuvutasigara na kukutanana mwanamke.Lakini yapomambo mengineyanayoharibuswaumu. Kwamaana unawezakushinda na njaa nakiu, lakini ukawahuna swaumu.”
Katikamafundisho yakeMtume (s.a.w)amesema kuwa-
“Yeyoteambaye hataachamazungumzomabaya na vitendoviovu, Allah (s.w)hana haja na kuachachakula chake nakinywaji chake.”
Na pia Mtumekasema katikanjia ya swali palealipouliza:
“Ni watu wangapwanafunga lakinihawana funga ilahuambulia kiu tu?”
Ni kwa kuzingatimafundisho hayo,Mtume (s.a.w)alipata kuwaamuruwatu wawiliwavunje funga zaokwa kuwa walikuwwakisengenya.
Pengine ili tuoneubaya wa kuteta nakusengenya watu,tuzingatie kisahiki. Wakati mmojaMtume (s.a.w)aliwakuta watuwakiwasengenya
wenzao, akawaita akaenda naokitambo kidogo wakakuta mzogawa punda. Mtume akawaamuruwale kidogo nyama ya mzoga ule.
Wote wakataharuki na kumshangaMtume kisha wakasema:
“Hakuna mtu yeyote anayewezakula nyama ya huu mzoga.”
Mtume (s.a.w) akawaambia, kosala kusengenya ni kubwa na bayazaidi ya kula mzoga huo.
Tukumbushane tena kauli yaMtume (s.a.w) aliposema kuwa:
“Mmoja wenu atakapoamkahali ya kuwa amefunga, asitumieau kusema kwa lugha chafu naasifanye matendo maovu. Na kamamtu yeyote atamchokoza au akatakkugombana naye, hana budikusema “Hakika mimi nimefunga”“Hakika mimi nimefunga.”
0719 434406/ 0783 509095
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
10/20
10 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 201Makala
MAMBO mazito kuhusupropaganda ya IS, yanazidikufichuka ambapo inabidisuala la kuchinjwa watundani ya Msikiti Mwanza,litizamwe kwa mapana yake.
Wakati huo huo, imeibukahali ya kushikana uchawibaina ya Saudi Arabia naMarekani, jambo ambalohalikutarajiwa. Hali hiyoinatoa funzo na kuthibitishakile kinachosemwa kila sikukwamba ‘Uncle Sam’ hanarafiki wala adui wa kudumubali masilahi yake.
“A DEMOCRATICCongressman (From CA!)
Admits ISIS Is Islamic”, ndivyoanavyoandika Robert Spencer(Mei 27, 2016) akisemakuwa mwakilishi Bradley
James “Brad” Sherman
wa Chama cha Demokratikutoka California, amekuwamwanasiasa wa kwanzakatika Marekani kusemawazi kuwa ‘ugaidi wa IS’ niUislamu na IS ni Waislamu.Na kwa maana hiyokinachotakiwa kupigwa vitani Uislamu.
Brad Sherman anasemakuwa Obama anapiga chengakutaja wazi kwamba ISni Uislamu na Waislamu.Akaongeza kusema kuwakatika kupiga chenga huko,Obama anadhani kuwaakionyesha unyama wa al-Baghdadi na IS kwa ujumlawakichinja watu, itawafanyavijana wa Kiislamu wasijiungena IS. Akasema, hiyo nidhana potofu kwa sababuwanaojiunga na IS wanaaminikuwa kuuwa ni katika Imaniya dini. Kwao kuuwa ni kiturahisi na cha kawaida na ndiokukamilika ‘ukhalifa’ wao.Akatoa rai kuwa kama mtuanataka kuwazuiya vijanawa Kiislamu wasijiunge naIS, basi atengeneze mkandawa video ukimuonyesha al-Baghdadi akila sandiwichi yanyama ya nguruwe.
Akifafanua mbunge huyoakasema kwamba mauwajikama yale dhidi ya kabilala Yazid na watu wengine(Masjid Rahman, Mwanza),haitawazuiya vijana waKiislamu kujiunga na ISkwa dhana eti kuwa huo sioUislamu. Bali watakachokionakuwa sio Uislamu labdawamuone kiongozi waoakila “ham sandwich”. Hamni nyama ya nguruwe, kwahiyo “ham sandwich”, nimkate uliowekwa nyama ya
Walio chinjwa Mwanza
Mazito yazidi kuibukaWasomi Saudia wazinduka usingiziniWaziri Mwinyi, huwezi kupigana na kivuli
Na Omar Msangi
nguruwe ndani.Akitilia nguvu kauli
yake, Bradley James “Brad”
BRADLEY James "Brad" Sherman.
Sherman anasema kuwa,kusambaza taarifa zaIS wakichinja Wakristo,
Cont. Pg. 11
hata Waislamu wasio IS,kutazidisha tu idadi yavijana wanaojiunga nakundi hilo. Akaongeza kuwahata kama kiongozi wa ISataonekana akila nguruwehadharani, bado Waislamuwatamfuata kama Amir
na Khalifah wao muda wakuwa anawaamrisha kuuwamakafiri na wanafiki wasiokuwa katika IS. Akachukua
baadhi ya Hadithi (Bukhari9.93.7142) alizodai kuwazinawahimiza Waislamukumtii kiongozi hatakama atakuwa muovu.Akahitimisha kwa kusemakuwa tatizo litakuwa tu paleal-Baghdadi atakapowaamurwafuasi wake kula nguruwemaana kuna aya zinakatazawaumini kufuata amri yakiongozi kama anaamuru
jambo la haramu, ila kiongoz
akifanya haramu yeyeafuatwe tu.
Tunachojifunza
Wiki iliyopitanilizungumzia juu yamlolongo wa matukioyaliyofuatana mpaka kutokeamauwaji ya Mwanza napicha inayojengwa ni kuwawaliohusika ni Waislamuwaliouwa Waislamu wenzaoNa kwamba wamefanya hivykwa kufuata mafundishoya Uislamu. Na ndio maanakila unapoambiwa kunamauwaji ya IS, basi kuna
bendera yenye Kalima yaShahada-Kalima ambayondio inamtoa mtu katikaUkafiri na kumuingiza katikaUislamu-Laa ilaaha ila llahuMuhammad Rasuulullah.”
Kwa muda mrefukumekuwa na malumbanomitaani na katika mitandaoya kijamii, juu ya ‘Salafi
Jihad’ waliokuwa wameibukna kuanza kutangaza
Jihad isiyo na mipaka kwamaana kuwa ya kuuwawasio kuwa Waislamu naWaislamu waliotangaziwaunafiki na ukafiri wakidaiwakuchelewesha Jihad nakusimama dola ya Kiislamu.Kule Mwanza watakumbukasana zilipoanza harakati za“Akina Abu Fulani” katika
baadhi ya Misikiti. Katikakulitizama jambo lile, sisitulisema kuwa lisitizamwekwa ufinyu. Haiwezi likawani jambo limejitokeza tu.Kuna mkono wa mtu nanguvu iliyopo nyumaambayo haionekani. Kule
Inaendelea Uk. 1
State sponsors of terrorismUS Planned and Carried out 9/11 Attacks…But Blames Other Countries for Them Out
By MEMRI - Middle EastMedia Research Institute
ON the eve of PresidentObama’s April 2016 visit
to Saudi Arabia, the U.S.Congress began debatingthe Justice Against Sponsorsof Terrorism Act (JASTA),that would, inter alia, allowthe families of victims ofthe September 11 aacks tosue the Saudi governmentfor damages. Also inApril 2016, the New YorkTimes published that a 2002congressional inquiry intothe 9/11 aacks had foundthat Saudi offi cials living inthe United States at the timehad a hand in the plot. Thecommission’s conclusions,said the paper, were specifiedin a report that has not been
released publicly.[1]The JASTA bill, which
was passed by the Senate onMay 17, 2016, triggered furyin Saudi Arabia, expressed both in statements by the
Saudi foreign minister and inscathing aacks on the U.S. inthe Saudi press.[2] On April28, 2016, the London-basedSaudi daily Al-Hayat publishedan exceptionally harsh articleon this topic by Saudi legalexpert Katib Al-Shammari, whoargued that the U.S. itself hadplanned and carried out 9/11,while placing the blame on ashifting series of others – firstAl-Qaeda and the Taliban, thenSaddam Hussein’s regime inIraq, and now Saudi Arabia.He wrote that Americanthreats to reveal documentsthat supposedly point to
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
11/20
11 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 20111 AN-NUU
MAKALA
Walio chinjwa Mwanza
Mazito yazidi kuibuka
Inatoka Uk. 10
Songea wakapita wenginewakichangisha pesa zakununulia AK-47 na risasi.Mtu unajiuliza, inakuwajemtu asimame katika misikitizaidi ya miwili anatangazawazi kuwa anachangisha pesa
za kununulia silaha, kimyaa!Huo ujasiri anaupata kutokawapi?
Vijana walilumbana sanakatika mitandao ya kijamiimpaka kutiana ukafiri. Baadaya propaganda kukolea nakuzungumzwa sana mitaanikauli za kujuzu kuchinjawanafiki na makafiri, sasayanakuja ya Mwanza nakauli za akina Bradley
James “Brad” Sherman,kwamba kuua ndio Uislamuwenyewe. Mtu ataonekana sioMuislamu kwa kula sambusaya nyama ya nguruwe, lakini
sio kuuwa mtu asiye na hatiakama walivyouliwa Waislamundani ya msikiti Mwanzaau waliochinjwa kule Tangamajuzi!
Katika hali hii kunamambo mawili ya kutizama.Moja ni lile walilosema“Masheikh” wa Saudia baadaya kukurupuka kutafutashuka wakati tayari ishatokaAdhana ya Alfajiri. Masheikhhao wanasema kuwaMarekani haiwezi kuishi bilaya kuwa na adui. Ilitengenezaadui ukomunisiti katikaVita Baridi, sasa imeugeukia
Uislamu kama adui wa dunia.Kwamba, baada ya
ukomunisti, alibuniwa adui‘Waislamu’ na ili adui huyoatishe, “masheikh” hawawa Saudia wanaizungumziaSeptemba 11, wakidai kuwa niMarekani yenyewe iliyopangana kutekeleza ikawasingiziaWaislamu ili kuudanganyaulimengu kuwa kuna ‘gaidi’wa kutisha-Waislamu.(Tazama: State Sponsors ofTerrorism: US Planned andCarried out 9/11 Aacks, butBlames Other Countries forThem Out-MEMRI - MiddleEast Media Research Institute)
Masheikh hawa wa Saudiawameibuka na kauli hizi
baada ya rafiki yao, mlinziwao wa kutegemewa,kuwageuzia kibao nakuwatuhumu kwamba waondio walipanga shambulio laSeptemba 11. Awali Saudiailiungana na Marekanikuwapiga Taliban/OsamaBin Laden (Afghanistan) nakisha Iraq ikidaiwa kwambaSaddam Hussein alikuwapamoja na Al-Qaida kupangashambulio la kimeta (anthrax
terror aack) na ndio sababuya kusingiziwa kuwa anasilaha za maangamizi. Baadaya Saudia kushirikishwa naMarekani katika vita yote
hiyo ambapo ilitoa mpakaardhi yake ili Marekani iwekekambi zake za kijeshi, sasainageuziwa kibao. Inaambiwandiyo iliyowadhamini
magaidi wale. Tarehe 17Mei, 2016 Bunge la Senetila Marekani lilipitishakwa kauli moja sheriainayojulikana kama “Justice
Against Sponsors of Terrorism Act” (JASTA) ili serikali yaSaudi Arabia ishitakiwena iwalipe fidia watu woteambao ndugu zao walikufakatika shambulio la Septemb11. Marekani inadai kuwaina ushahidi wa kutoshakwamba Saudi Arabiailiwasaidia kwa kuwapapesa na kuwawezesha kwakila namna magaidi 19walioteka ndege 4 na kufanyshambulio la kigaidi katikaardhi ya Marekani Septemba11, 2001.
Ni baada ya kugeukwahuko, sasa Wasaudiawanaibuka na kuishutumuMarekani kwamba inapangaugaidi na kuutekelezayenyewe ili ipatekuwasingizia watu wengine.(Tazama: 9/11 Disinformation:Saudi Arabia Aacked America-By Paul Craig Roberts.)
Mpaka sasa sio wazi, niniMarekani inataka katikasarakasi hizi mpya za kurasa28 za siri (28 pages classifiedsecret) zinazoituhumu SaudiaArabia na ujio wa JASTA. Je,ni kutaka tu mapesa ya bureau ina mpango wa kuipigakama ilivyoipiga Afghanistanna Iraq kwa kisingizio hichohicho cha ugaidi. Hata hivyo
la kujifunza hapa ni kuwa,hata kama tutajifanya wemavipi na watiifu kiasi ganikatika ‘kutumiwa’-kuwawashirika wa kuaminikakatika vita dhidi ya ISna ugaidi kwa ujumla,tukaandaa mikutano kuleArusha, mazoezi ya pamojaya kijeshi na mambo kamahayo, jamaa wakitaka jambolao ambalo pengine mkakatiwake ni kugeuziwa kibaokama Saudia inavyofanyiwahivi sasa, wala Uncle Samhataona aibu wala kuhisivibaya kutufanyizia. Wala sis
hatujawa vipenzi kwa ‘UncleSam’ kama wafalme waArabuni!
Katika kuhitimisha Makalahaya, lipo jambo moja lakuhoji. Baadhi ya vyombovya habari vimemnukuuWaziri wa Ulinzi na Jeshi laKujenga Taifa, MheshimiwaDr. Hussein Mwinyi akidaikuwa nchini kuna mtandaowa kigaidi wa Al-Qaida na ISWaziri Dk. Hussein Mwinyi,alidai “kuwepo kwa mitandahiyo (ISIS na Al-Qaida) tena
From Pg. 10
Inaendelea Uk. 1Cont. Pg. 13
WANAODAIWA Alshaabab katika mapango ya Amboni, Tanga.
State sponsors of terrorismSaudi involvement in 9/11 arepart of standard U.S. policy ofexposing archival documents touse as leverage against variouscountries – which he calls“victory by means of archives.”
Following are excerpts fromAl-Shammari’s article:[3]
”Those who followAmerican policy see that itis built upon the principle ofadvance planning and futureprobabilities. This is because itoccasionally presents a certaintopic to a country that it doesnot wish [to bring up] at thattime but [that it is] reservingin its archives as an ace to play[at a later date] in order topressure that country. Anyonerevisiting… [statements by]George H.W. Bush regardingOperation Desert Storm might
find that he acknowledgedthat the U.S. Army could haveinvaded Iraq in the 1990s, but that [the Americans] hadpreferred to keep SaddamHussein around as a bargainingchip for [use against] otherGulf states. However, once theShi’ite wave began to advance,the Americans wanted to get ridof Saddam Hussein, since theyno longer saw him as an ace uptheir sleeve.
“September 11 is one ofwinning cards in the Americanarchives, because all the wisepeople in the world whoare experts on American
policy and who analyze theimages and the videos [of9/11] agree unanimously thatwhat happened in the [Twin]Towers was a purely American
action, planned and carried outwithin the U.S. Proof of thisis the sequence of continuousexplosions that dramaticallyripped through both buildings…Expert structural engineersdemolished them withexplosives, while the planescrashing [into them] only gavethe green light for the detonation– they were not the reason forthe collapse. But the U.S. stillspreads blame in all directions.[This policy] can be dubbed‘victory by means of archives.’
“On September 11, the U.S.aained several victories at thesame time, that [even] the hawks[who were at that time] in theWhite House could not have
imagined. Some of them can beenumerated as follows:“1.The U.S. created, in public
opinion, an obscure enemy –terrorism – which became whatAmerican presidents blamedfor all their mistakes, and also became the sole motivationfor any dirty operation thatAmerican politicians andmilitary figures desire to carryout in any country. [The]terrorism [label] was appliedto Muslims, and specifically toSaudi Arabia.
“2. Utilizing this incident[9/11], the U.S. launched a
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
12/20
12 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 20112 SAFU YA BEN RIJAL
Na Ben Rijal
Jee, tujichore miili yetu?
JAMII mbalimbali kujichora rangi katika miili yao
UISLAMU umewawekea mapambozaidi wanawake na wanawakendio wa kuwa kwenye mapambo,mwenye kuvutia na kumvutiamume ni mwananmke na ndiowakahalalishiwa kuvaa dhahabu,mwanamume ni haramu kuvaadhahabu. Aidha, mwanamume niharamu kwake kuvaa herini lakinimwanamke hayo ndio mapamboyake, mwanamke kujipaka hinaamependekezwa mwanamumeana mipaka ya kupaka hio hina.La kupendeza na kuvutia wanja ni
pale anapoutia mwanamke.Uislamu umeharamishamwanamume kujinasibishakama mwanamke na mwanamkekujinasibisha kwa vivazi vyakiume, ingawa wanawake miaka hiiwanavaa suruali, hutakiwa wazivaekwa dharura na wasivae kwamtindo wa kuonyesha umbo lakena kuwa ni mvuto kwa wanaume.
Kuingia chochote kile kwenyengozi ya Muislamu hutakiwa mtuajitahidi kukiondoa iwe lami,ubani, rangi n.k. kwani udhuunatakiwa ukae kwenye ngozi yamwenye kutia udhu wala sio juuya rangi nyengine iliopo juu yangozi. Mola muumba ametuumbakwa kujua yupi amuumbe kwenyerangi ipi, iwe nyeusi, maji ya kunde
na rangi ilio sio nyeusi sio majiya kunde kwani hakuna ranginyeupe kama tunavyosema autunavyoitakidi watu weupe, kwanirangi nyeupe tunaijua kwa hiohakuna mtu mwenye rangi nyeupe.
Wanadamu wote kwa maumbileMola kawaumba kwa mfumommoja, anapotafautiana mmojawetu kuwa na rangi hiii au ilesio jengine ila ni kitu kinaitwa“Melanin” na hii ndio inajaaliauwe mweusi au rangi nyengine nakuwa na nywele za mlalo au tuzitekama huko nyuma zilivyokuwazikiitwa singer, hizo ni protiniinayojengwa na aina ya amino acidijulikanayo cysteine na cystine,leo mtu anaweza kuzigeuzanywele zake kutoka nywele zakibantu na kuja kuwa na nywele
za singer lakini hayo huwa ni yamuda, kwani hio njia ya vitu viwilihivyo hutengenezwa na kufanyakiunganishi dhaifu kwenye nywele,kiunganishi hicho baada ya mudahuvunjika na kumfanya aliowekahio dawa atie dawa nyengine nahayo ni ya kujirejea, baya zaidinikuwa kila siku zikisonga mbelenyewele hizo hukatika.
Jamii mbalimbali kujichora rangikatika miili yao
Kujipaka rangi na chimbuko lake
Kujiremba rangi katika miiliya watu, rangi ambayo baada yakujichora huwa haitoki ila kwanjia ya upasuaji. Uchorwaji wa
KATIKA makala iliopita nilikuwa najaribu kuelezea uvazi waKata “K” na hasara zake. Aidha chimbuko lake, kwa kweli ikiwahatujui chimbuko la mambo kama hayo na kwanini yameshamirikatika miaka yetu hii, ukweli itakuwa ni hasara. Hivi sasakumeshamiri uchorwaji wa miili ya rangi kwa watu maarufuhasa wachezaji wa michezo, kwa Kiengereza inajulikana kama“Taoos”. Uchorwaji huu umejizatiti hasa na wachezaji wa mpirawa kikapu kule nchini Marekani NBA na watu wa sanaa na hivisasa imekuwa haina simile kwa wachezaji wa mpira kwenye ligi yaUiengereza ijulikanayo kwa jina EPL. Lakustaajabisha kuna vijanawa Kiislamu ambao nao wamejiingiza katika kujichora. Hao nikina Soule Muntari kijana wa Kiislamu kutoka nchi ya Ghana naOzil kijana mwenye asili ya Kituruki na raia wa Ujerumani.
MESUT Ozil mchezaji wa Arsenal na Tatoo.
Taoo sio jambo la juzi wala janaupakaji huu wa kujichora rangini wa dahari na haukuwa katikaeneo moja la dunia hii tunayoishiila uchoraji wa rangi katika miiliulikuwa na unafanyika hadi sasakila mwahali duniani na ushahidihuu umejionyesha katika maitizilizohifadhiwa za watu wa Firauniwa Misri. Aidha, baadhi ya sehemu
za Ulaya nyakati za Paleolithiczimeonekana vyombo ambavyovikitumika kuchorwa miili ya watu.
Uchorwaji wa Taooumethibitika kuwa ulianza tangumiaka 4 ya millennium kabla yakuzaliwa kwa Nabii Issa AS. Katikafukua na kuangalia tamaduni zawatu waliopita katika miaka bainaya 3,370 na 3,100 kabla ya kuzaliwakwa Mtume Issa AS watu wa OiIceman walikuwa wakijichora naithibati hio imeonekana kufukuliwamaeneo yasiopungua 49 katikamaeneo ya nchi za Greenland,
Alaska, Siberia, Mongolia, Sehemuza Magharibi ya China, Misri,Sudan, Philippines na Andes.
Kuweza kuelewa haya ya
kujichora mwili Taoo tumsomeDaktari Lars Krutak ambayeamefanya utafiti juu ya Taoo naasili yake zilivyoanza. DaktariKrutak amechukua muda wakemwingi kutembea kwenye mabarambalimbali na nchi mbalimbalikutaka kujua juu ya uchorajiwa aina mbalimbali za pichakatika miili ya watu. Kitu kimoja
alichokuja kukigundua ni kuwa jamii mbalimbali katika mataifambalimbali yakijichora kwamintaarifu ya kujitambulisha,kutambika, wanawake kuwavutiawanaume, alama za kuashiria jambo na wengine ni alama zaimani za dini zao za asili.
Katika utafiti wake DaktariKrytak lilomshangaza ni kuonawengine wakiwachora wakezao kwenye midomo iwe nikivutio na kuwatia hanjam palewanapowaona. Katika maitiiliohifadhiwa na kuwekewamadawa katika nchi ya Marekaniya Kusini, aidha Daktari Krutakalishuhudia maiti yenye umrimkubwa inayofikia miaka 6,000kabla ya kuzaliwa Mtume Issa
AS maiti isiokuwa na alama yamasharubu, badala yake sehemu ykuota masharubu imekolezwa kwmchoro wa Taoo.
Vyombo vya kuchoreaTaoo vimegundulikana kuwahavipishani na vinavyotumikamiaka hii, ila tu kinachopishana nikuwa vinavyotumika miaka hii nivya kisasa na muda unaochukuwakuchora ni mdogo kuliko wa miakya nyuma. Huko nyuma pichaya kuchorwa iwe kwenye mkonoau kifua inaweza kuchukua sikunzima kuchorwa.
Mlolongo wa uchorwaji waTaoo ni mrefu na kuna haja yakuulezea kwa kina namna watuwanavyojichora na kwanini
wanajichora na jee kuna atharigani ya Taoo kiafya na Uislamuunasemaje juu ya Taoo.
Fatana na mie kwenye makalaijayo juu ya michoro ya pichakatika miili yetu, juu ya hayo yotenitapendekeza vijana wa Kiislamuambao wameanza kujitokezakujichora na wengine kujiwekeazile za muda kuwashauri kwaharaka waache kufanya hayo nawajisomee kuelewa dhambi yamichoro hii katika Uislamu. Jambo jema watu wajifunze na kuelewadini yetu inavyotufunza na kupatasomo, lipi ni halali na lipi niharamu?
Tusikubali kuyahalalisha matuskuwa Waislamu hawasomi wakatiaya ya mwanzo alioteremshiwa
Mtume (SAW) ni soma-Iqra nakusoma ndio utamaduni waKiislamu na Waislamu walifikambali kutokana na kusoma.
MESUT Ozil akiwa Umrah.
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
13/20
13 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 201MAKALA
Walio chinjwa Mwanza
Mazito yazidi kuibuka
Inatoka U. 11
kwa kuwatumia vijana waKitanzania kutekeleza azmayao ovu kwa rai.”
Alitoa madai hayo “wakatiakiwasilisha makadirioya mapato na matumiziya bajeti ya Wizara yakekwenye Bunge la Bajeti mjiniDodoma, Mei mwaka huu.”
Ndivyo alivyonukuliwaWaziri Mwinyi na gazeti la
Jibu la Maisha. Jambo la kuhoji hapa ni
hili: Ushahidi wa kuwepoISIS nchini ni upi? Je, nizile picha za vijana watatuwalio katika mlango wapango wakiwa na benderanyeusi? Kama ni hizo, je, tokaakina David Paul Goldman,
jamaa zao wa ‘A Gay GirlIn Damascus’ , wasambazepicha hizo, Polisi wetu na
JWTZ yetu na vitengo vyake,wameshindwa kuwakamatavijana hao au kuwafurushakatika mapango hayo? Aundio Waziri wetu Mwinyinaye anataka kuwaleteaWatanzania ‘usanii’ wa “BringBack Our Girls” kwambavijana hao watatu waliovaliayebo yebo, ni magaidi hatarikiasi kwamba Polisi wetuna JWTZ wetu hawanaubavu wa kukabiliana nao?Tuwaombe radhi Polisiwetu na JWTZ kwa swalihili kwa MheshimiwaWaziri, hatukusudii
kuonyesha wasiwasi juu yauwezo wa vyombo vyetuhivyo muhimu, bali nikatika kujenga tu hoja nakuchukua tahadhari tusijetukatumbukizwa katikamitego ya propaganda zamabeberu, tukampa mwanyaadui kuendeleza maovu yake.
Mheshimiwa WaziriMwinyi, kama walivyosemawataalamu, watafiti nawachambuzi wengi, ugaidisi adui, bali ni mkakatiwa mabeberu wa kufikiamalengo yao. Mtu kutangazakwamba ana mikakati
na mipango ya kipolisi,kikachero na ki-JWTZ yakupambana na kushindaugaidi wa Al-Qaida, AlShabaab na sasa IS, ni sawana kujidanganya yeyemwenyewe. Utapambanavipi na adui asiyeonekana?Utapigana vipi nakumshinda adui kivuli?Kama hilo linawezekana, leotusingekuwa tunasikia habariza Abubakar Shekau, Nigeria.
Madai mengine kamahaya ya Mheshimiwa WaziriMwinyi, ni kumpa tu adui
From Pg. 11
nguvu zaidi ya kutubamiza.Huu ndio uzoefu kutoka nchinyingine unavyoonyesha.La kusikitisha ni kwambahatujifunzi. Tumekuwa watu wakukimbilia mashua inayozamawakati waliomo ndaniwakitapatapa kutaka kujinuru.
Nigeria iliimbishwa, ikaimba
kwa juhudi na maarifa kwambakuna magaidi wanaitwa BokoHaram wakiongozwa naAbubakar Shekau, matukio yakupanga ya hapa na pale yakawyanatokea huku ikiimbwa kuwani Boko Haram. Ilipokubalikapropaganda hiyo, sasa serikalina nchi nzima Nigeria,imekuwa kichekesho na kiroja.Wanatekwa wasichana mia tatuwanafichwa katika msitu wa“Kazi Mzumbwi”, miaka mitatupolisi, jeshi la nchi, makachero nusaidizi wa nje, bado kinatambakibwagizo cha “Bring Back OurGirls” kilichoanzia WashingtonD.C.
Boti tunayosema kwambainazama, ni kule wewekukubali kuimbishwa nakukariri propaganda kuwanchini mwako kuna magaidi.Wimbo ukishakolea, huna lakufanya. Utapigwa na walahutamjua anayekupiga ni nani.We utabaki tu kuimba wimbowako uliokaririshwa kuwa kunamagaidi wa IS na Al-Qaida!
Sasa kauli hizi za kuparamiapropaganda za uwepo IS kwakutegemea kauli za kulishwana akina David Paul Goldmanna picha zao za kutengenezakwenye komputa za vijana na‘buti za yeboyebo’ kwamba etindio ushahidi wa kuwepo IS na
Al Qaida, ni kutaka kutuingizakatika boti inayozama walikoNigeria, Kenya, Pakistan nawengine.WAZIRI wa Ulinzi, Dkt. Hussein Mwinyi.
State sponsors of terrorismnew age of global armament.Everyone wanted to acquireall kinds of weapons to defendthemselves and at the sametime bale the obscure enemy,terrorism – [even though] upto this very moment we donot know the essence of thisterrorism of which the U.S.speaks, except [to say that] thatit is Islamic…
“3. The U.S. made theAmerican people choosefrom two bad options: eitherlive peacefully [but] remainexposed to the danger of death[by terrorism] at any moment,or starve in safety, because [thecountry›s budget will be spenton sending] the Marines evenas far as Mars to defend you.
“Lo and behold, today, wesee these archives revealed before us: A New York courtaccuses the Iranian regime ofresponsibility for 9/11, and we
[also] see a bill [in Congress]accusing Saudi Arabia of being behind it [sic]. This is afterthe previous Iraqi regime wasaccused of being behind it.Al-Qaeda and the Taliban werealso blamed for it, and we donot know who [will be blamed]tomorrow! But [whoever it is],we will not be surprised at all,
since this is the essence of howthe American archives, that arecivilized and respect freedomsand democracy, operate.
“The nature of the U.S. isthat it cannot exist without anenemy… [For example,] aftera period during which it didnot fight anyone [i.e. followingWorld War II], the U.S. createda new kind of war – the ColdWar… Then, when the Sovietera ended, after we Muslimshelped the religions and foughtCommunism on their [theAmericans›] behalf, they beganto see Muslims as their new
enemy! The U.S. saw a needfor creating a new enemy – andplanned, organized, and carriedthis out [i.e. blamed Muslims foterrorism]. This will never enduntil it [the U.S.] accomplishesthe goals it has set for itself.
“So why not let theseachievements be credited to theAmerican administration, whileinsurance companies pay forthe damages, whether domesticor foreign? This, my dear Araband Muslim, is the policy of theAmerican archives.”
Notes:[1] Nytimes.com, April 15,
2016.[2] See MEMRI Special
Dispatch No. 6397, AgainstBackdrop Of Obama’s VisitTo Riyadh: Saudi, Gulf PressFurious At Allegations Of SaudiInvolvement In September 11Aacks, April 21, 2016.
[3] Al-Hayat (London), April28, 2016.
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
14/20
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
15/20
15 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 201SAFU YA BEN RIJAL
MGENI tukimsubiri kwa mwakamzima na sasa ameshafikana mgeni anatakiwa sikuzote afanyiwe maandalizi naakishafanyiwa maandalizihungojewa apokewe nakutimiziwa kila kilichokuwakizuri.
Ramadhani ni mwezi ambaouliteremshwa Qur’an “Enyi mlioamini! Mmeandikiwa Saumu, kamawaliyo andikiwa walio kuwa kablayenu ili mpate kumcha mungu.”(2:183)
Katika aya hii, ni wazikabisa tunaambiwa kuwatumefaradhishiwa funga yaRamadhani kama kaumumbalimbali zilizopata kupita nakufanyiwa haya sio kama ni uonevuwala kitu chengine chochote kile,ila kuweza kupata “Taqwa” yaanikumcha Mungu.
Haikuwa kumcha Mungu nikwa Ramadhani tu, ila kumchaMungu ni kwa miezi yote kwayule aliokuwa Muislamu yupo
baligh na akili timamu, mtu huyoatatakiwa amche Mungu miezi yote11 isipokuwa hii Ramadhani niChuo ambacho kinamchukua mjana kumtakasa kisha kumpelekeakatika miezi 11 ilio baki awekama alivyokuwa ndani ya mweziwa Ramadhani. Ramadhani niChuo chenye kutoa mafunzokwa waja na mafunzo yake huwamja hasimamiwi ila hujisimamiamwenyewe.
Utukufu unapatikana kwakumcha Allah na kujitolea kwakokuyawacha mabaya na kufwata yalealiokuja nayo Mtume Muhammad(SAW):
“Enyi watu! Hakika Sisitumekuumbeni kutokana namwanamume na mwanamke. Natumekujaalieni kuwa ni mataifana makabila ili mjuane. Hakikaaliye mtukufu zaidi kati yenu kwaMwenyezi Mungu ni huyo aliyemcha mungu zaidi katika nyinyi.Hakika Mwenyezi Mungu niMwenye kujua, Mwenye khabari.”(18:17).
Funga kwetu sio mzigo kwanifunga huwa ni siku chache mnokatika mwaka “(Mfunge) sikumaalumu za kuhisabika. Na atakayekuwa miongoni mwenu mgonjwaau yumo safarini basi atimizehisabu katika siku nyengine. Nawale wasio weza, watoe fidiya kwakumlisha masikini. Na atakayefanya wema kwa kujitolea, basi ni bora kwake. Na mkifunga ni borakwenu, kama mnajua.” (2:184).
Funga haijamtia kambamuumini anapokuwa na dharuraya ugonjwa wala akiwa safarini,kisha tukatakiwa kwa walewasioweza watoe fidiya. Funga
ukifwata alivyofunga Mtume(SAW) na masahaba hali yako yakiafya itatengenea, Mtume (SAW)katufahamisha kwa kauli “Fungenimtapata siha.”
Utukufu wa mwezi waRamadhani ni mkubwa mno,kwani una usiku ulio bora kabisaambao ni usiku wa Laylatul qadri“Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'anikatika Laylatul Qadri, Usiku waCheo Kitukufu.” (97-1), “Na ninikitacho kujuulisha nini LaylatulQadri?” (97-2), “Laylatul Qadrini bora kuliko miezi elfu.” (97-3),“Huteremka Malaika na Rohokatika usiku huo kwa idhini yaMola wao Mlezi kwa kila jambo.”(97-4), “Amani usiku huo mpakamapambazuko ya alfajiri.”
Tuiangalie miezi alfu ndani ya
Salamu zangu za mwezi mtukufu wa Ramadhani kwenu
Nakutakieni Ramadhani njema na ya amani
usiku mmoja, mwezi ukiwa nasiku 30 na mwaka ukiwa na siku365. Aidha miezi 12 ina mwakammoja. Hesabu ya haraka harakaukichukua 1,000/12 utapata 83.3yaani ni miaka 83.3 ni sawa na miezi1,000 ambayo imo katika usikuhuu mtukufu ambao ni mmoja tuna haupo kwenye mwezi wowoteule isipokuwa Ramadhani, hii nizawadi kubwa wamepewa watuwa Umma wa Mtume Muhammad(SAW) ambao wanaishi umrimdogo.
Usiku wa Laylatul qadri niusiku mkubwa na usiku huutunatakiwa tuufanyie kazi yakikwelikweli. “Naapa kwa Kitabukinacho bainisha” (44:2), “Hakika
tumekiteremsha katika usikuulio barikiwa. Hakika Sisi niWaonyaji” (44:3), “Katika usiku huuhubainishwa kila jambo la hikima.”(44:4).
Mwezi huu ni mwezi ambao“Mashetani hufungwa katikamwezi huu” (Bukhari). Mashetaniwanaotupelekea kufanya maasi,verejee iwe Ramadhani na weweunafanya maasi, hapo nikusemakuwa mja wa sampuli hio yupo juuzaidi ya Shetani.
Kuna mambo tunatakiwa natumependekezwa kuyafanyakwa mwenye kufunga nayoni, kuharakisha kufuturu,kuchelewesha kula daku nakujiepusha na kusema mambomachafu, watu wengine huonani udaruweshi mwadhini wamagharibi kuadhini na kutotakakula chochote kile hadi amalize
kusali, "Watu hawataacha kuwakatika kheri wakiwa wanaharakishakufuturu". (Imehadithiwa na AlSheikhan). Tunatakiwa jua likichwana muadhini akiadhini, basi hapohapo tuhakikishe tunafunguakinywa na vyema tufungue kwatende. Hio ni suna na utumie kwanjia ya witri (odd number) yaanikwa nambari zisogawika kwa 2 iwe1, 3, 5, 7, 9, 11 n.k. Wengine husemamaeneo yetu tende hazipatikaniau ghali, basi ukikosa tende uanzekufungua kinywa kwa kitu kitamuau maji, wengine siku hizi hufunguakwa chokoleti, hapo unakosa sunakama alivyokuwa akifanya MtumeMuhammad (SAW) ikiwa yeye nikigezo chetu.
Jambo la pili ni kucheleweshakula daku na tule daku walau kwa
kitu kidogo. Haijakuwa kula dakuni njia ya kuongeza uzito. Daku nisehemu ya kukufanya uwe na akibaya kukupa nguvu ya kufanya kaziwakati upo kwenye funga, lakininalo hilo daku lisiwe zito kamauswahilini watu walivyo kuliwakwa wali wa nazi, mchuzi, mbogana matunda, unatakiwa ule kwakiasi. Madaktari wa kimamboleowanatufundisha kuwa daku zuri ulevyakula vya nafaka kwani husagwapolepole na kukuwezesha kupatanguvu, kuliko daku la vitu vyamajimaji mfano wa boga, mumunyan.k.
Jua fika kuwa Funga itakukingiakifua siku ya Ramadhani “Fungaitasema Ewe Mola nimemkinga mja
huyu kwa kujizuia kula na kunywana matamanio mengine sio kwa jengine lolote lile ila kwa ajili yako.”
Lolote lile katika kufanikisha jambo hutakiwa uwe na mpangouliojipangilia (Plan) na mienitakuambia mpango wako uwe:
i) Kaa itikafu khasa katika kumila mwisho, ii) Kumi la mwisho nasiku za kuanzia tarehe 21 jitahidikuitafuta Laylatul qadri na hayani kwa kukaa Msikitini itikafu nakusoma Qur’an na ikiwa hutowezakuwepo Msikitini, basi ujifungenyumbani kwa kusoma Qur’an nakumsalia Mtume (SAW) kwa wingi,iii) Kithirisha kusoma “Allahummainnaka ‘afuwwun, tuhibbul-‘afwa,fa’fu ‘ann,.” iv) Toa sadaka kwawingi hata kokwa moja ya tende nisadaka, v) Usipende kufakamia nakula katika vyungu 7 na ziada, juafika kila utapokula sana na uvivu
utakuvaa,vi) Kuwa mtu wa mfano kwakutenda mema na atakayekukoseana kughadhibika na weweusishindane naye umwambie “mienimefunga, ” vii) Usipoteze wakatiwako kwa mambo yasio kuwana maana kama kucheza karata,dhumna, drafti, keram, kuangaliavideo kwa wingi na mengineo yaanasa viii) Wafuturishe Waislamuwenzako, kwani Fadhila ya mwenyekumfuturisha Muislamu mwenzakeni sawa na thawabu anazopatamja aliofunga, ix) Wahimize walionyumbani mwako na walio karibuna wewe kufanya mambo mema, x)Usiwache suna ya kusali Tarawehena Witri, xi) Hudhuria darasa zatafsiri za Qur’an, xii) Ukiowaonavijana wamekuja kusali na hawasali
siku nyengine kuwa karibu naona kuzidi kuwashajiisha bila yakuwapa maneno ya kuwavunjamoyo. xiii) Tujiweke mbali namatamanio ya mwili na hata kwawale waliokuwa halali na sisi,uhalali unaanza baada ya kuzamakwa jua, xiv) Jitahidi kutafutariziki ya halali kwani sawmu zetuzitakwenda ajwar kwa kula vitu vyharamu, xv)Tusipoteze wakati wamchana kwa kuuchapa usingizi.
xvi) Kithirisha kusoma Qur’analau juzuu moja kwa siku. NakupaFormula rahisi, ikiwa juzuu mmojaina kurasa 15, basi na wewe ukiwaunasali sala 5 kila siku, kwenyekurasa 15 zigawe kwa 5, 15/5=3,kwa hio kila baada ya sala ukisomakurasa tatu kwa siku utapata juzuummoja, ukisoma kurasa 6 kila baada ya sala utasoma juzuu 2 kwasiku na ukisoma kurasa 9 utakuwaumesoma juzu tatu kwa siku. Jeeunajua kwa wastani mtu anasoma juzuu mmoja kwa dakika 30?
Jee unajua mpira wa miguu
huchezwa kwa dakika ngapi? Nidakika 90. Kwa hiyo kile kipindiunachotizama mpira kwa dakika90, ufahamu kuwa una uwezo wakusoma juzuu 3 za Qur’an na ikiwakutafika na wakati wa nyongezayaani “Extra time” dakika 120,itakufanya kuwa umesoma Juzuu4. Nikuulize hujawahi kuangaliampira unaokwenda hadi dakika120? Itavyokuwa jawabu yakoujuwe unapoangalia mpira dakika120 ni sawa na kusoma Qur’an juzuu nne.
xvii) Jitenge na simu yako yamkononi kuitumia nje ya umuhimuwa kupiga au kupigiwa, jitengekwa kadri uwezavyo na “Internet” jiweke mbali na Mitandao ya jamii,iwe Face book, Whatsapp, Skype nmengineo, sema ku-chat Ramadhaiwe mchana iwe usiku kwangu nimwiko na nitafanya kama kuna haya kufanya hivyo.
Hakika mwezi huu ni mweziambao unakupa taswira kubwaya Umoja wa Kiislamu, kwaniutapokwenda popote pale kwenyedunia hii utayaona munayoyafanyhapa na kwengine nako hufanywakama muyafanyao, iwe kula vizurikusali tarawehe, kusali witri, kuwawanyenyekevu, kutoa sadaka kwawingi n.k.
Nakuomba na kukuzinduaMuislamu mwenzangu unapokuwkatika funga, kaa kila marauwaombee Waislamu wenzakowalioingia katika mtafaruku wavita na kutojuwa nini watachokilawala hawatojuwa vipi watakuwawanafanya ibada kwa utulivu.Waislamu hao ni kutokaAfghanistan, Yemen, Iraq, Syria,Palestine, Libya, Somali, Afrika ya
Kati na kwengineko. Kila wakatiiwe inatupitikia katika nafsi zetu juya shida wanazokumbana wenzetukatika nchi hizo nakumuomba Allaawapatie ufumbuzi kwa mashakayaliowazonga yawaishie kwa marammoja.
Tuwaombe wenzetuwanaokwenda Umra kwenyemwezi huu wawaombee wenzetuhao na watuombee na sisi tupateamani na utulivu na kutafutamachumo ya halali.
Salamu zangu hizi kwangukwako ziwe za mkono kwamkono na wewe mpelekee salamumwengine na iwe hivi hivi.
Ewe Mola tufikishe Ramadhanikwa salama na amani na tuwewenye afya na tuweze kutimizaibada vilivyo. Ameen.
8/15/2019 ANNUUR 1232.pdf
16/20
16 AN-NUU
SHAABAN 1437, IJUMAA JUNI 3 - 9, 201Makala
MWAKA 1964, kulitokeaMaasi ya Jeshi yaliyodaiwakuwa lengo lake ni kutakakumuondoa kwenye Urais,Mwl. Julias K. Nyerere, ambayealirudishwa katika madarakayake na jeshi la Uingerezalililoletwa maalumu kumalizamaasi hayo. Baada ya halikutulia, kitu kilichofuatia nikamata kamata ya Masheikhna baadhi ya Viongozi wengiwa iliyokuwa Jumuiya yaUhisani ya East African MuslimWelfare society [E.A.M.W.S] nakuwekwa kizuizini kwa madaiya kwamba nao walishirikikatika kupanga mpango waMaasi hayo. Kadhia hiyo
ilipofikishwa kwenye vyombovya sheria, hakuna hata mmojawao ambaye alipatikana nahatia ya kushiriki kwake katikampango huo. (Chanzo: M. Said(2002)).
Katika ile OperesheniMaalumu ya kusakwawaliodaiwa “Eti” ni MAGAIDI,Wilayani Kilindi-Tanga.Mnamo mwaka 2013., ambapokadhia hiyo ilipelekea baadhiya Waislamu kupotezamaisha, kupatwa na vilemavya kudumu, kufunguliwamashitaka, wazazi kupoteana nafamilia zao, watu kuangamiziwamali zao n.k. hatimaye Kadhia
hiyo ilipofikishwa Mahakamaniwalionekana hawana hatia nakuachiwa huru. (Chanzo: Annuur Julai 4-10, 2014.)
Kuachiwa huru kwa AbuHutheifah aliyedaiwa ni Gaidi:
Hebu soma hii: “In May 2003,local police offi cers accompaniedby American FBI offi cers, arrestedand detained without charge ortrial, Shaykh Ramzi Faraj or AbuHudhaifa, the Director of the Al-Haramain Islamic Foundation,and Shaykh Ahmed Said Abry, theDirector of Dhiy Nureyn (Iringa).”
“New York Times of July 7,
2006, the FBI took Shaykh AbuHudhaifa from Tanzania to Afghanistan where he was heldincommunicado for 16 months.He has since been released. In July2004”. (Chanzo: Hamza Njozi(2012) BJTRP Volume 4 Number 1December 2012.)
Maana:Mwezi Mei 2003, maafisa
wa polisi wa Tanzaniawakiongozana na Marekanimaafisa FBI, kukamatwana kuwekwa kizuizini bilakushitakiwa au kuhukumiwa,Sheikh Ramzi Faraj au Abu
Ugaidi au propaganda kuhujumu Waislamu?Na Abu Saumu, Kombo
Hassani Kidumbu.
Hudhaifa , Mkurugenzi wa Al-Haramain Islamic Foundation,na Shaykh Ahmed Said Abry,Mkurugenzi Dhiy Nureyn(Iringa.)
Kwa mujibu wa gazeti laNew York Times la Julai 7,2006, FBI ilimchukua ShaykhAbu Hudhaifa kutoka Tanzania
na kupeleka Afghanistanambako aliwekwa kizuizini kwamuda wa miezi 16. Na yeyekutolewa. Mnamo Julai 2004(bila kufunguliwa na mashitakayoyote na kuthibishwa ugaidiwake). (Tafsiri isiyokuwa rasmi).
Aliyekuwa Waziri wa Mamboya Ndani, Bw. Ali Ameir wakatihuo, alisema:
“Serikali ina taarifa ya kuwepokwa kundi la vijana wanaopewamafunzo rasmi ya kuendelezafujo nchini kwa kisingizio chadini”. (Maneno hayo aliyatoakwa wakati wa kadhia ya mauaji
ya Waislamu Mwembechai1998-Chanzo: Nipashe Februari19, 1998.)
Aliyekuwa Waziri Mkuu waTanzania (2001) Bw. FrederickSumaye naye alisema:
“Serikali ina taarifa kuwakuna kundi la vijana wa CUFlililokuwa nje kujifunza vitendovya ugaidi…..kuna hata
mipango kuwadhuru viongozi,kulipua taasisi (muhimu) namiundo mbinu na majengo”.(Chanzo: Nipashe Januari 26,2001.)
Rais Mkapa kwenye hotubayake kwa taifa aliyoitoa Februari3, 2001, alisema:
“Hatuigopi CUF kwenyeulingo wa siasa wala hatuogopiugaidi wao…………………….”(Chanzo: Annuur toleo laFebruari 6-8, 2001 uk.10)
Kama vile ambavyoulimwengu uliaminishwa
juu ya kitisho cha Neo-Nazi,na ndiyo ambavyo hivi sasaulimwengu umeaminishwa juuya kitisho cha ugaidi. Akina
Mislovan Kouba wa zama zetunao wamejipenyeza kwenyesafu zetu na kuwa “BrainWash” Waislamu kiasi ambacho“WATAHEMKWA” na kutumikkuuangamiza imani, mali nanafsi wa ndugu zao katikaimani kwa dhana ya kwambani kuipigania dini. Au wakatimwingine kina Kouba hutumiafursa ya kuleta (ugomvi) bainaya Waislamu kwa kupandikizafitna kwa kufanya tukio lahujuma (ugaidi) dhidi yakundi moja, na kuenezwapropanganda kwamba hujumahiyo imefanywa na kundi jinginla kiislamu na kutengezwa“Drama”. Hivyo kundi hilolitaanza kushughulikiwa kwakubamizwa viongozi na harakazake.
Matendo ya kigaidi naujambazi ni mambo mabayaambayo athari zake hazichaguimtu, dini, dhehebu, taasisiau chama fulani. Na kwamsingi huo, ugaidi na magaidiau Ujambazi na Majambaziwanastahiki kupingwavita. Hivyo mtu akitakakukuangamiza hukutengenezeatuhuma za Ugaidi au Ujambazi
kwa kuundia mazingira ambayyataweza kuiaminisha jamiikwamba wew